PIUMA KUHUDHURIA MKUTANO WA TANGO- MBEYA
PIUMA imewakilisha ASASI zote ambazo si za kiserikali za wilaya ya makete katika mkutano wa TANGO .MKUTANO huo uliambatana na mafunzo kwa waliohudhulia , mafunzo kwa ujumla yalikuwa ni kuzijengea ASASI uwezo wa kushiriki katika mambo mbalimbali yanayo fanyika katika Halmashauri , moja ya mada ambazo zilifundishwa zilikuwa ni pamoja kushiriki katika kupisha bajeti ya halmashauri , kushiriki katika kufanya tathimini ya huduma za jamii katika wilaya, Hivyo basi kwa mafunzo hayo PIUMA ina nafasi ya kupeleka wajumbe wawili katika kamati ya kufanya tathimini ya huduma za jamii wilani makete ,wajumbe hao wata ambatana na wajumbe wengine ambao nao walipata mafunzo haya. Kamati imejumuisha madiwani, wataalamu toka halmashauri, wajumbe toka asasi mbalimbali, pamoja na watu raia toka kwenye vituo ,Hata hivyo katika mkoa wa Iringa Mjumbe kutoka PIUMA ndiye alipendekezwa na asasi za mkoa huo kuhojiwa na waandishi wa hahari ili kuelezea matatizo ambayo asasi zinayapata huko kwenye maeneo yao.
Kwa pamoja tutashinda.
