Archive for August, 2009

Friday, August 28th, 2009

PIUMA BUIDING TO DATE

slowly we can!

upper floor

upper floor

 

windows and door flem
windows and door flem

Friday, August 28th, 2009

Makete waanza kulima Pareto

Na Evance Seth.

 

Wananchi wilayani Makete wamekuwa na furaha tena baada ya zao la biashara la Pareto kuanza kununuliwa tena. Pareto ni zao pekee la biashara Wilayani Makete  lilitoweka baada ya kukosekana kwa soko.

 

Akizungumza na mwandishi wa habari hii mmoja wa wakulima wa zao hili Bwana Kensi alisema ”Nimeanza kulima zao hili mwaka 2007 baada ya kupata nguvu kutoka kwa  kampuni ya pareto walipokuja kijijini kwetu na kutuahidi soko la uhakika’’

 

Wanunuzi hao wa pareto wanatoa motisha na uhamasishaji kwa wakulima kulima kwa wingi zao hili kwa kuwapunguzia gharama za ukulima kwa kugawa mbegu bure kwa wanakijiji wakulima. Mbegu ambazo zimekuwa zikipatikana kwa watendaji wa vijiji bure hutolewa bila urasimu wote.

 

Bw. Kensi mmiliki wa shamba la ekari moja anavuna pareto yake kila wiki na hutumia siku tatu kukauka wakati wa kiangazi na wiki moja wakati wa msimu wa mvua. Aliendelea kusema bei ya kilo moja ya pareto ni sh. 900/= kwa hiyo kwa mwezi huwa anakusanya kilo zisizopungua arobaini.

 

“Nikishakausha pareto yangu huipeleka kwa Afisa kilimo ambapo hupimwa na kupewa pesa zangu keshi”. Alisema Bw. Kensi.

 

Kilimo cha pareto ni kilimo rahisi sana kwani hakihitaji mbolea na matunzo makubwa zaidi ya palizi inayofanywa mara mbili kwa mwaka. Na zao linalompatia mkulima pesa kila wiki.

 

Hata hivyo Bwana Kensi alisema kuwa matatizo madogo madogo ambayo huwa anayapata hasa wakati wa masika pareto hukuchukua muda mrefu kukauka kwani jua huwa linakuwa la shida, na mvua zikinyesha mfululizo husababisha pareto hiyo kuoza, na biashara yake kuwa sio nzuri.

 

‘’Pamoja na kuwa biashara sio nzuri malengo yangu ya baadaye ni kuongeza kulima mashamba mengine ya pareto, kwani pesa ninayopata inanikwamua kwenye matatizo madogo madogo ya kifamilia”alisema Bw. Kensi.

 

Ulimaji wa zao la preto ulistawi kuanzia miaka ya 1960 na kusimama miaka ya 1980 baada ya matumizi ya DDT kupigwa marufuku na hivyo pareto ambayo ilikuwa malighafi ya dawa hiyo kukosa soko.

 

Ingawa wakulima wa Makete hawajui pareto inatumika kwa ajili ya nini sasa, lakini wanashukuru kwasababu hivi sasa soko la Pareto limekuwa zuri kwani imeshaanza kupata soko kwenye soko la dunia.

Bwana Kensi akiwa anachuma pareto.

Bwana Kensi akiwa anachuma pareto.

Friday, August 28th, 2009

Upimaji wa Aridhi

Na Evance Seth

 

Wilaya ya Makete imeungana na wilaya zingine za Tanzania katika zoezi la kitaifa la upimaji wa Aridhi na viwanja. Zoezi hili linaratibiwa na kuendeshwa na Mpango wa Kurasimisha Rasimali na Biashara za wanyonge Tanzania (MKURABITA).

 

Akizungumza na mtandao huu mwenyekiti wa kijiji cha Iniho Bw. Ferance Sanga alisema zoezi hili limeanza katika wilaya ya Makete mwezi April. Hata hivyo Bw. Sanga alisema mvua zilizokuwa zikinyesha wakati wa masika zilipunguza kasi ya upimaji wa viwanja na mashamba.

 

Alipohojiwa na Mtandao huu kama anaona faida zozote za zoezi hilo Bi. Roda Muhando alisema, upimaji unawasaidia watu kuwa na hati ya umiliki wa mali zao. “kukatia hati miliki hiyo ni faida kwako kwani hakuna mtu atakaye kupokonya  shamba lako kwani utakuwa umekatia hati miliki na litatambuliwa ni la kwako” aliongeza Bi. Muhando.

 

Bi. Roda aliwaasa wanawake kujitokeza kwa wingi kupewa hati za kumiliki mashamba na Viwanja  kwani inawapa nguvu wanawake. “Nikiwa mwanamke nashukuru Serikali kwa kuanzisha huu mpango kwani sasa sitanyanyaswa kutokana na jinsia yangu kwenye umiliki wa aridhi” aliendelea kusema Mama Muhando.

 

Pamoja na zoezi la upimaji shirika pia litasaidiana na wanachi kujenga ofisi kwa ajili ya matumizi ya maofisa wa kijiji, baraza la aridhi na maofisa wa aridhi. Katika ujenzi huo wananchi watachangia nguvu, uwanja na mawe kwa ajili ya ujenzi na gharama zingine zote zitagharamiwa na MKURABITA.

haya ni baadhi ya mashamba yaliyopimwa.
Sehemu ya Mashamba yaliyopimwa Kijijini Bulongwa

Picha na Witness

Thursday, August 13th, 2009

Vijana wapewa stadi za maisha

Na Evance Seth

 

Wakati vijana wa kijiji cha iniho wakiendelea na semina nyingine kijijini kwao kama ilvyoripotiwa na mtandao huu, vijana wengine wa umri kati ya miaka kumi na nne hadi kumi na nane walikuwa wakipata elimu nyingine ya stadi za maisha kijijini Bulongwa.

 

Katika semina iliyofanyika ukumbi wa Dinduka kijijini Bulongwa iliratibiwa na wakufunzi Salum Sanga, afisa utamaduni wa wilaya ya Makete na Bw. Juma Sanga, afisa utamduni wa wilaya ya Makete iliwashirikisha vijana kutoka katika vijiji vyote vya tarafa za magoma na Bulongwa.

 

Vijana wawili kutoka katika kila kijiji walifanya jumla ya vijana sitini walioshiriki semina hiyo waliowawakilisha vijana wenzao wa kata nne za tarafa hizo mbili za Bulongwa na Magoma. 

 

Wakizungumza na mtandao huu kutoka katika ukumbi wa semina hiyo Vijana Mary Baghdad wa Iniho na Joseph Muvela wa kijiji cha Iyoka walisema “Hii semina ilikuwa na nia ya kuwapa vijana nyenzo za kukabiliana na mazingira hatarishi ya maambukizi ya UKIMWI”

 

“Tumejifunza namna ya kukabiliana na mihemko, mahusiano, kuwa wabunifu, ushirikeli na kujitambua,” walisema vijana hao. Wakizungumzia stadi ya kujitambua vijana hao walioungwa mkono na wenzao waliokuwa wamewazunguka wakati wa mahojiano na mwandishi walisema, stadi hii ni muhimu kwani inamfanya kijana ajijue anatoka wapi, yupo wapi , anafanya nini na anakwenda wapi.

 

Bw. Salum Sanga alisema wamefanya mafunzo na vijana walio chini ya miaka kumi na tisa kwasababu vijana wa umri chini ya miaka kumi na tisa wengi wao hawajapata nafasi ya kupata elimu ya stadi za maisha wakiwa nje ya mashule.

 

“Vijana wengi wa umri huu wametoka mashuleni hivi karibuni kwa hiyo kuna ulazima kuwapa elimu inayofanana na mazingira wanayoishi sasa, mazingira ya nje ya shule” alisema mkufunzi wa semina hiyo Bw. Sanga. Vijana hao wanategemewa kuwa mabalozi na kutoa elimu kwa vijana wenzao vijijini wanakotoka.

 

Vijana wakipata semina ya stadi za maisha

Vijana wakipata semina ya stadi za maisha

 

 

 

Thursday, August 13th, 2009

Vijana na UKIMWI

Na Evance Seth

 

Wiki hii vijana wapatao ishirini wa kijiji cha Iniho wamefaidika na elimu juu ya ugonjwa wa UKIMWI. Elimu iliyotolewa katika semina iliyowashirikisha vijana kuanzia miaka kumi na tano.

Akizungumza na mwandishi wa habari hii mkufunzi wa semina hiyo Bw. Maonyesho Ngohani alisema semina hiyo ililenga kuwajengea uwezo vijana hao  wa kuweza kukabiliana na changamoto mbali mbali zinazoambatana na maambukizi ya virusi vya UKIMWI.

“UKIMWI huleta madhara kwa mtu binafsi, familia yake na jamii kwa ujumla kwa hivyo ni muhimu kuwapa vijana nyenzo  na stadi za maisha kuweza kukabiliana na madhara hayo” alisema Bw. Ngohani. Mada nyingine iliyotolewa ilikuwa ni pamoja na namna ya kuwatunza walioathirika na VVU pamoja na kuondoa Unyanyapaa.

Akizungumzia sehemu za stadi za maisha za kuwakinga na VVU vijana Bw. Ngohani alieleza kuwa vijana hawana budi kujishirikisha na michezo, pia kushiriki katika shughuri za kimaendeleo zitakazo wainulia vipato vyao. Alisema ajira kwa vijana, vifaa na viwanja ya michezo ni changamoto mojawapo inayowakabili vijana katika kushiriki kikamilifu kwenye mapambano ya VVU.

“Tunawashauri vijana kuendelea kushikiria na kufuata ABC za kuepuka maambukizi ya VVU” alisema Mkufunzi huyo. Akizitaja ABC hizo bwana Ngohani alisema vijana lazima wajiepushe na Ngono, wawe waaminifu kwa wapezi wao na kutumia kondomu kila wanapofanya tendo la ngono. “Kila mtu ana mchango katika mapambano dhidi ya UKIMWI” alimalizia Bw. Ngohani.

 

“Vijana tunahitaji kujitambua na kujua umuhimu wetu katika mapambano dhidi ya UKIMWI” alisema Eva Lufingo mmoja wa washiriki wa semina hiyo. Akifafanua zaidi kijana huyo alisema vijana wana nyenzo na uwezo wa kutokomeza UKIMWI na kuasa jamii kuwa iwape nyenzo na nafasi ya kushiriki kwenye mapambano ya dhidi ya UKIMWI

Monday, August 3rd, 2009

Kitulo - Matema Tourism

By Evance Seth

The Kitulo national park for the first time last week has received biggest number of fifteen tourist at one time from Europe. Although Tanzania is a country with large and beautiful national park and reserve as Serengeti and Selous Kitulo is of its kind.

Unlike other national parks which are rich of animals, Kitulo is a national park with thousands of flower species and is a resting point of bird when flying from the northern pole to the southern pole.

Speaking through their translator these tourists said they were very much impressed by the beauty that they have experienced in Kitulo national park which they called it a natural garden.

On their way to Matema beach the Tourist made a camp in Iniho Village at Ivala grazing plateau. Mr. Allain Mbilinyi who was coordinating this trip from Iniho said Ivala is a communal land put aside for grazing. “Since waking are no longer rearing large groups of cattle we can convert this place into a camping site and become more useful” said Mr. Mbilinyi

Ivala is a mid way from Kitulo to Matema beach of Lake Nyasa via the Livingstone ranges with Kitulo being 3000 meters above sea level and Matema beach at Lake Nyasa 1.5 below sea level. The two places are separated with walking time of two days with good vicinity on the way including the Kapunji animals which are one of the extinct creatures on earth found in forests around Livingstone ranges.

Apart from the natural beauty experienced, the the tourist said that they were also impressed by people life in the villages on their way, the life of peace and respect with each other including clean and good environment.

When talking to this website one of the youth who was helping carrying luggage of the tourists said for youth it mean business as they make some money from helping the tourists with their luggage. “It is like a temporary employment for me and my fellow young men” commented the young man.

 

Tourists camping at Ivala, Iniho for a night break before they could proceed to Matema the next day

Tourists getting ready to walk down slope of more than 2500M to Matema beach

Photo by Evance