Thursday, August 13th, 2009

Vijana na UKIMWI

Na Evance Seth

 

Wiki hii vijana wapatao ishirini wa kijiji cha Iniho wamefaidika na elimu juu ya ugonjwa wa UKIMWI. Elimu iliyotolewa katika semina iliyowashirikisha vijana kuanzia miaka kumi na tano.

Akizungumza na mwandishi wa habari hii mkufunzi wa semina hiyo Bw. Maonyesho Ngohani alisema semina hiyo ililenga kuwajengea uwezo vijana hao  wa kuweza kukabiliana na changamoto mbali mbali zinazoambatana na maambukizi ya virusi vya UKIMWI.

“UKIMWI huleta madhara kwa mtu binafsi, familia yake na jamii kwa ujumla kwa hivyo ni muhimu kuwapa vijana nyenzo  na stadi za maisha kuweza kukabiliana na madhara hayo” alisema Bw. Ngohani. Mada nyingine iliyotolewa ilikuwa ni pamoja na namna ya kuwatunza walioathirika na VVU pamoja na kuondoa Unyanyapaa.

Akizungumzia sehemu za stadi za maisha za kuwakinga na VVU vijana Bw. Ngohani alieleza kuwa vijana hawana budi kujishirikisha na michezo, pia kushiriki katika shughuri za kimaendeleo zitakazo wainulia vipato vyao. Alisema ajira kwa vijana, vifaa na viwanja ya michezo ni changamoto mojawapo inayowakabili vijana katika kushiriki kikamilifu kwenye mapambano ya VVU.

“Tunawashauri vijana kuendelea kushikiria na kufuata ABC za kuepuka maambukizi ya VVU” alisema Mkufunzi huyo. Akizitaja ABC hizo bwana Ngohani alisema vijana lazima wajiepushe na Ngono, wawe waaminifu kwa wapezi wao na kutumia kondomu kila wanapofanya tendo la ngono. “Kila mtu ana mchango katika mapambano dhidi ya UKIMWI” alimalizia Bw. Ngohani.

 

“Vijana tunahitaji kujitambua na kujua umuhimu wetu katika mapambano dhidi ya UKIMWI” alisema Eva Lufingo mmoja wa washiriki wa semina hiyo. Akifafanua zaidi kijana huyo alisema vijana wana nyenzo na uwezo wa kutokomeza UKIMWI na kuasa jamii kuwa iwape nyenzo na nafasi ya kushiriki kwenye mapambano ya dhidi ya UKIMWI

Leave a Reply