Thursday, September 10th, 2009

WANAPIUMA WAKUSANYIKA KUMKARIBISHA DR. ZIN ZIN.

 Na Witness ngumba.

 

Juzi tarehe 08/09/2009 ulifanyika Mkutano wa kumkaribisha Dr. zin zin na wanachama wa PIUMA pamoja na uongozi wao, mkutano huo ulifanyikia  kwenye jengo la PIUMA. Jumla ya wanachama waliohudhuria walikuwa 80 idadi hii ni kama nusu ya wanachama wote,  wanachama wengine walishindwa kufika kutokana na sababu mbalimbali walizotoa kwa katibu.

 

Akizungumza na mwandishi wa habari hii Katibu Mkuu wa PIUMA  Bi. Anna Mwinuka “alisema kuwa ujio wa Dr. Zin Zin ni mzuri kwa sababu ameshaanza kufanya kazi na wanaPIUMA kama kuhudumia wagonjwa kwa utafiti wa ndani, hivyo wagonjwa wanaendelea kufarijika na kumiminika kwa kasi kwenda kituoni kupima afya zao kutokana na uwepo wake PIUMA. Amesema kuwa yupo  tayari kutufundisha wanaPIUMA kiingereza pamoja na kuanzika kwa kutumia Kompyuta. Na kwa nyuso za wanachama wengi walionyesha kufurahia ujio wake huyu daktari kwani siku hiyo baada ya kujitambulisha kwa jina la Dr. Zin Zin na kueleza malengo yake ya kuja PIUMA ni kufanya kazi na PIUMA hasa kwenye masuala ya afya, wanachama walifurahi na kuimba nyimbo kwa shangwe na vigelegele.

 

Kwa niaba ya wanaPIUMA wote tunapenda kutoa shukrani zetu kwa wale wote walioshiriki katika mchakato wa kumtafuta daktari huyu na hatimaye kumsafirisha na kufika PIUMA  kwani tumetambua kuwa tunapendwa na wafadhili  na mnautambua umuhimu wa afya zetu”alisema Katibu”.

 

WanaPIUMA wakisubiri mkutano kwenye jengo lao.

WanaPIUMA wakisubiri mkutano kwenye jengo lao.

Dr. zin Zin akizungumza na wanaPIUMA

Dr. zin Zin akizungumza na wanaPIUMA

 

WanaPIUMA wakiimba na kutawanyika.

WanaPIUMA wakiimba na kutawanyika.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

5 Responses to “WANAPIUMA WAKUSANYIKA KUMKARIBISHA DR. ZIN ZIN.”


  1. royal orr says:

    Thank you, Witness, for the report and photos! Veru much appreciated. And karibu sana to Dr. Zin Zin. I know she will make an enormous difference in our work together.

    Royal
    Canadian Friends of Highlands Hope


  2. Jackson says:

    Kwa Pamoja Tushinda, Daima mbele msirudi Nyuma! Hongera PIUMA, Karibu Dr. Zin Zin,


  3. Fabian Wirnsperger says:

    Yippee, PIUMA has a new doctor!!!!!!!!! The one and only in Bulongwa ;-)


  4. Rainer Brandl says:

    Dr. Zin Zin from Myanmar is a very kind and educated physician. She studied Tropical Medicine at Mahidol University in Bangkok and did a special training in HIV/AIDS treatment in a Bangkok clinic.
    I truly hope and wish for her, that she can work free of hassles and can help PIUMA to show full accountability and good use of resources.
    Zin Zin comes from an environment in a country like Myanmar, which is certainly “poorer” than Tanzania and gets less “help”.
    I believe that she can contribute a lot for people in Tanzania, who mostly suffer under corruption and theft of resources.
    She can teach, train, educate and show people that there is no need to die from HIV/AIDS and many other diseases. In case you do the right thing.
    All the best Zin Zin!


  5. malila says:

    Let us give her time and cooperation,this will enable her to deliver what she has.

    Hongereni kwa kupata dakitari.

Leave a Reply