Archive for October, 2009

Thursday, October 29th, 2009

RAIS JAKAYA KIKWETE ATEMBELEA KATA YA BULONGWA AKIELEKEA MKOA WA MBEYA.

Na Witness Ngumba.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika ziara ya kutembelea mkoa wa Iringa ametembelea kijiji cha Bulongwa leo mnamo saa 4:30 asubuhi akielekea mkoa wa Mbeya.

Alipofika katika kijiji cha Bulongwa njia panda Namanga, alikumbana na mkusanyiko wa wanakijiji wa bulongwa, wanafunzi pamoja na wanachama wa PIUMA wakiwa kati kati ya barabara wakitaka kuonana na Rais.

Rais alimwomba mwenyekiti wa kijiji cha bulongwa ili aweze kuzungumza nae kwa niaba ya wanakijiji wote ili atoe matatizo yanayowakabili wananchi wa kijiji hiki.

Mwenyekiti wa kijiji cha Bulongwa Bw. Merikizedeki Jekela alisema kuwa tatizo la kwanza ni mbolea za ruzuku hazifiki kwa muda mwafaka na zikifika  haziwafikii walengwa. Rais alisema kuwa tatizo hili amelipata kwa vijiji vingi na ameshaongea na viongozi wa Wilaya juu ya kutatua tatizo hili.

Tatizo la pili  ni mawasiliano ya barabara alimweleza Rais kuwa bara bara yetu wakati wa masika huwa inaharibika na kusababisha kukosekana kwa mawasiliano ya bara bara. Rais alisema kuwa hili tatizo ameliona na alivyokuja mwaka jana aliwaagiza viongozi wa Wilaya ya Makete waanze kutengeneza barabara kwa lami kuanzia Njombe hadi Makete, alisema kuwa amepitia kuangalia utekelezaji huo na ameona wameshaanza utengenezaji wa barabara hiyo, lakini alisema kuwa kwa barabara ya Bulongwa kwenda Mbeya atapitia kuiangalia na kuona ni jinsi gani ya kuikarabati.

Tatizo la tatu ni maji ya bombani, mwenyekiti alimweleza Rais kuwa tulikuwa na maji ya bombani ambayo yalitengenezwa na DANIDA miaka ya nyuma sana lakin kwa sasa vifaa vya maji vimechakaa, na kusababisha maji kushindwa kuwafikia wananchi wa Bulongwa, alimwomba Rais ukarabati wa mradi huo ili wananchi waendelee kupata maji. Rais alisema kuwa alimepokea hilo lakini uongozi wa kijiji uandike madai hayo na kupeleka kwa uongozi wa Wilaya ili wao wapeleke kwenye uongozi wa mkoa na hatimaye taifani ukiwafikia wao wataangalia ni jinsi gani ya kuwasaidia wananchi wa Bulongwa.

 

Tatizo la nne Umeme; Mwenyekiti alimweleza Rais kuwa kijiji cha bulongwa mto Luvanyina ambao unaweza kuzalisha umeme sasa mheshimiwa atatusaidije juu ya hili. Rais alisema kuwa alishawahi kupata habari za mto huo, kwa hiyo bado wanaufanyia kazi.

 

Wananchi wa Bulongwa walifurahi sana kuweza kumfahamu Rais na kuweza kuwasikiliza matatizo yao na Rais mwenyewe alisema kuwa amefurahi sana kuweza kuonana nao kwani kupita vijijini ndipo anapogundua matatizo mengi ya wananchi, baada ya hapo aliwaaga wananchi na kuondoka kuelekea mkoa wa Mbeya.

Rais Jk akiongea na Mwenyekiti wa kijiji cha Bulongwa

Rais Jk akiongea na Mwenyekiti wa kijiji cha Bulongwa

 

 

 

wanaPIUMA wakiwa miongoni mwa kumpokea Rais

wanaPIUMA wakiwa miongoni mwa kumpokea Rais

 

wananchi wamekusanyika wakimsubiri Rais

wananchi wamekusanyika wakimsubiri Rais

 

 

 

 

Tuesday, October 27th, 2009

Ujenzi wa Sekondari Iwawa

Na Evance Seth

 

Wananchi wa kata ya Iwawa wanakabiliwa na shughuli  za ujenzi  wa  majengo yanayoendelea kujengwa shuleni hapo  ikiwa pamoja na  ujenzi wa Hosteli , Maabara , Maktaba pamoja na  jengo kwa ajili ya kidato cha tano na kidato cha sita.

 

Hayo  yamezungumuzwa na  Afisa mtendaji  wa Kata  ya Iwawa Bw Selemani Kiwone katika mazungumzo yake na mwandishi wa habari hii.

 

Akizungumzia ujenzi huo mkuu wa shule hiyo Bw.  Omath Sanga amesema kuwa wananchi wametoa mchango  mkubwa  katika ujenzi unaoendelea kwa usombaji  wa mawe, mbao, uchimbaji kiwanja pamoja na  mafundi kujenga majengo hayo.

 

‘’viongozi wa serikali wanatakiwa kutambua  umuhimu  kushiriki kikamilifu katika shughuli za ujenzi” alisema Bw. Kiwone. Akifafanua juu ya suala hilo Bw. Kivone alisema katika ujenzi wa shule za ya sekondari  baadhi ya viongozi wa Halmashauri wapo nyuma  katika kuchangia  ujenzi. “Hali hiyo inasababisha  kuwakatisha tama wananchi wanaotoa michango pamoja na nguvu zao shuleni hapo” alimalizia Bw. Kiwone.

 

Naye mkuu wa shule ametoa changamoto zinazo wakabili shuleni hapo kuwa ni pamoja na upungufu wa walimu, nyumba za walimu, baadhi ya vyumba vya madarasa kuto karabatiwa na kusababisha wanafunzi kulundikana katika darasa moja, hali ambayo ina sababisha mwalimu kushindwa kufanya kazi kwa ufanisi.

Sunday, October 25th, 2009

We are Hope

 

PIUMA

PIUMA

Ari Mpya, Nguvu Mpya kwa Pamoja Tutashinda!
Ari Mpya, Nguvu Mpya kwa Pamoja Tutashinda!

 We are proud to be part of the great army that battles HIV/AIDS on the field. We are one Army under one comander “HOPE”

Friday, October 23rd, 2009

Wagoma kuzika maiti

Na Mwandishi wetu

Jeshi la polisi  kituo cha matamba  limewakemea  wananchi wa Tarafa hiyo  kuacha tabia  ya Imani potofu  pindi  kifo cha mtu kinapo tokea  hasa katika mazingira ya kutatanisha.

 

Kauli hiyo imetolewa na  na Jeshi hilo kutokana na wananchi wa kijiji cha Lugoda kilichopo kata ya Mlondwe kuweka mgomo  kuto mzika  mkakazi  mmoja wa kijiji hicho Bi Salai Nkwama  kwa kile kinacho sadikika  kuwa mama huyo amefariki kwa imani za kishirikina.

 

Uchunguzi uliofanywa na madaktari kituo cha afya  cha Matamba , imeonekana mama huyo haja fariki  kwa imani za kishirikina  wanavyo zani wanajamii wa kijiji hicho.

 

Kwa upande wao wananchi  wamesema kifo  cha Bi. Salai kimetokea usiku  wa kuamkia  ambapo  mama huyo aliugua  ghafla na kukimbizwa kituo cha afya  Matamba  ambapo alifariki muda  mchache baadaye.

 

Hata hivyo wananchi hao wamesema endapo serikali kutolifumbia macho suala la  watu wenye imani za kishirikina  kwani kama serikali haitakemea tatizo hilo ndio mwanzo wa uvunjifu wa amani na haki za binadamu.

 

Hivi karibuni kumekuwa na upigaji kura zoezi liloendelea nchi nzima kuwabaini watu wanaojihusiha na vitendo vya mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi “albino”  Habari za uhusika wa ganga wa jadi na imani za kishirikina kwenye mauji hayo zilifichuliwa na mwandihishi mwandamizi wa BBC nchini Bi. Vicky Ntetema.

 

“Unajua hata vita dhidi ya UKIMWI inakuwa ngumu sana kama tutaendelea kusadiki kuwa watu wanauawa kichawi” alisema Bw. Kambanyuma mwenyekiti wa PIUMA alipokuwa akitafakari pamoja na mwandishi wa habari hii.

Friday, October 23rd, 2009

Matumizi ya Benki Yaongezeka Makete

Na Evance Seth

 

Meneja wa NMB tawi la Makete Bi. Doris  Luvanda amesema kumekuwa na ongezeko kubwa la wateja wa Benki hiyo katika msimu wa Januar hadi machi kwa mwaka huu 2009.

 

Bi. Luvanda ameyasema hayo wiki iliyopita alipokuwa akizungumza na na mwandishi wa habari hizi kuhusu hali ya ongezeko la wateja pamoja na huduma na huduma zitolewazo na Benki ya NMB tawi la Makete.

 

Aidha amesema kuwa wateja wote waliokuwa wamejaza fomu kwa ajili ya kupata kadi za ATM, kadi zao zimekwisha wasili tangu mwezi wa pili mwaka huu. Hata hivyo Bi. Luvanda alitoa angalizo kw wateja watakao chelewakuchukua kadi zao, “atakayechelewa kuchukua kadi hizo ndani ya miezi sita atatakiwa kuomba upya na atalazimikakulipia gharama za kadi upya yaani kamisheni” aliongeza Bi. Luvanda.

 

Akielezea hali ya watu waliofariki wakati wakiendesha akaunti zao katika Benki hiyo amewaomba ndugu wa marehemu kufika katika benki hiyo ili kupata maelezo ya kina na namna ya kupata pesa katika akaunti za marehemu hao.

 

Bi. Luvanda amewataka wale wote waliofungua akaunti katika benki hiyo na kukaa zaidi ya mwaka mmoja bila bila kuweka wala kuchukua fedha, hivyo kusababisha akaunti zao kulala wanatakiwa kufika na picha za paspoti size ili kufufua akaunti zao.

 

Kumekuwa na ongezeko kubwa la utunzaji wa pesa kwa wanachi wa Makete hivi karibu, Vijana wengi wamekuwa wakitunza pesa zao benki.

Friday, October 23rd, 2009

Vijana Makete Kusoma Ufundi

Na Evance Seth

 

Mkurugenzi mkuu wa VETA nchini Bwana. Zebadia Moshi akiwa ameongozana na baadhi ya wakurugenzi wa VETA nchini mwezi uliopita walikabidhiwa rasmi na uongozi wa Halmashauri ya Wilaya Makete mkataba wa kuanza kujengwa kwa chuo cha VETA wilayani Makete.

 

Akizungumza na Kitulo FM mwezi uliopita Bw. Moshi alisema kuwa mpango wa serikali ni kujenga vyuo 126 kwa awamu tatu katika wilaya zote hapa nchini, ambapo awamu ya kwanza vitajengwa vyuo thelathini, na Wilaya ya Makete ikiwa imepewa nafasi ya kwanza Kitaifa kuanza ujenzi wa chuo cha VETA.

 

Aidha  ameishukuru Halmashauri ya Wilaya ya Makete kwa utekelezaji wa kutafuta hatimiliki pamoja na maandalizi ya miundo mbinu ya mahali kitakapojengwa chuo hicho.

 

Naye Mkuu wa Wilaya ya Makete Bi. Hawa Humbi na mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya Mh. Ona Amosi  Sikunala Nkwama amesema kuwa kujengwa kwa chuo hicho kutasaidia vijana wa Makete kupata elimu ya ufundi kwani mbao zinazouzwa nje ya wilaya zitaboreshwa kwa kutengeneza vifaa bora vitakavyouzwa ndani na nje ya Wilaya.

 

Jumla ya shilingi Bilioni tatu zimetengwa kwa  ajili ya ujenzi wa chuo hicho kitakachokuwa kinatoa fani mbalimbali za ufundi.

Tuesday, October 6th, 2009

A Month in Dar Es Salaam

         

  

  By Dr Zinzin Winkoko,

   PIUMA volunteer doctor

”I am on my second day in Tanzania, I have been studying Kiswahili language, the main language spoken in this country, necessary for me for working in this Country as volunteer medical doctor.

  

I am supposed to study 20 hours according to the schedule for beginner course. Because of the limited time, I could not join to group section which is normally open per period but I have a chance to study in special class.


Therefore, every day but Sunday, I have been studying 3 hours per day. Moreover I decided to extend one extra hour a day, for a total four hours every day, given the short duration of my course…Studying language for four hours in a special class, it is not what you could call it a good method but I have to do when it is happening.

 

It is quite tiring after studying 2 hours because absorbing quality of my brain is becoming poor. Especially, 2 hours lesson after lunch time is a tough job. 

 

According to Tanzanian culture, greeting is very important and the people are proud of greeting before doing anything. So, it has been such a difficult issue for me even to buy drinking water in the early days here.


On the other hand, it really takes me time, the lady doctor who come from Burma (Myanmar), South East Asia, to be ready and not to be shocked when a stranger appear suddenly willing to greet, even though I know the proverb that says “when in Rome do as Romans do!”. I really regret and feel sorry for my late replies to their sincere and friendly greetings!!!

  

Another issue is for the food: I am the one who loves Asian food like papaya salad, other spicy food and Myanmar traditional food called “Mont Hin Khar” . Not only in Myanmar, but also in Thailand I was used to that food for one year. It is hard now to get familiar with African food, especially stiff porridge called “Ugali”. Sweet tea every early morning is a similar custom like in my home town, but those who don’t have that habit still need to be trained.

  

It shouldn’t be left about the bus called “Daladala” when talking about Dar Es Salaam. There are too much crowed in the bus in office hours in my country, but ladies, are first priority usually according to our custom.


We, ladies, old people and children, have been comfortable in the bus while travelling also. Because of cost effectiveness, we have been trying to take the bus from the bus station called “Mwenge” which is not so far from the place we are staying. After waiting for a while, a median size bus that is going to downtown was coming, and there was also crowded in office hour like our country exception with no priority to ladies here. And then, I was really surprised when something was happening unexpectedly, but I was trying to cope with the habits of that city. Somehow, I still like that city.
 

 

Sincerely, I was afraid of dogs since I was in childhood and never imagine staying for one month at the house with six dogs. But finally, these days makes me a part of duty to buy some biscuits for them, to make them friendly. Incredibly they even became some days I would never forget about.

 

After 2 week studying time, I have a chance to practice around the campus such as in shopping center, restaurant and music center around Nyum Ba Ya Sanam which is the place where I used to studying. However, studying one language within 3 weeks made me crazy sometimes, and I did had bad mood on the way back to the place I stayed and even thought I should give up.
But in reality I did not!!!! 

 

Finally, Days passed by very quickly, and I came to the night before I am going to leave for IRINGA . I wish I could come back to that beautiful city to meet with native friends from Dar Es Salaam and wish to chat by Kiswahili.”

zinzin winkoko during her swahil training at Dar Es salaam-Tanzania

zinzin winkoko during her swahil training at Dar Es salaam-Tanzania