Friday, October 23rd, 2009

Wagoma kuzika maiti

Na Mwandishi wetu

Jeshi la polisi  kituo cha matamba  limewakemea  wananchi wa Tarafa hiyo  kuacha tabia  ya Imani potofu  pindi  kifo cha mtu kinapo tokea  hasa katika mazingira ya kutatanisha.

 

Kauli hiyo imetolewa na  na Jeshi hilo kutokana na wananchi wa kijiji cha Lugoda kilichopo kata ya Mlondwe kuweka mgomo  kuto mzika  mkakazi  mmoja wa kijiji hicho Bi Salai Nkwama  kwa kile kinacho sadikika  kuwa mama huyo amefariki kwa imani za kishirikina.

 

Uchunguzi uliofanywa na madaktari kituo cha afya  cha Matamba , imeonekana mama huyo haja fariki  kwa imani za kishirikina  wanavyo zani wanajamii wa kijiji hicho.

 

Kwa upande wao wananchi  wamesema kifo  cha Bi. Salai kimetokea usiku  wa kuamkia  ambapo  mama huyo aliugua  ghafla na kukimbizwa kituo cha afya  Matamba  ambapo alifariki muda  mchache baadaye.

 

Hata hivyo wananchi hao wamesema endapo serikali kutolifumbia macho suala la  watu wenye imani za kishirikina  kwani kama serikali haitakemea tatizo hilo ndio mwanzo wa uvunjifu wa amani na haki za binadamu.

 

Hivi karibuni kumekuwa na upigaji kura zoezi liloendelea nchi nzima kuwabaini watu wanaojihusiha na vitendo vya mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi “albino”  Habari za uhusika wa ganga wa jadi na imani za kishirikina kwenye mauji hayo zilifichuliwa na mwandihishi mwandamizi wa BBC nchini Bi. Vicky Ntetema.

 

“Unajua hata vita dhidi ya UKIMWI inakuwa ngumu sana kama tutaendelea kusadiki kuwa watu wanauawa kichawi” alisema Bw. Kambanyuma mwenyekiti wa PIUMA alipokuwa akitafakari pamoja na mwandishi wa habari hii.

Leave a Reply