Wagoma kuzika maiti
Na Mwandishi wetu
Jeshi la polisi kituo cha matamba limewakemea wananchi wa Tarafa hiyo kuacha tabia ya Imani potofu pindi kifo cha mtu kinapo tokea hasa katika mazingira ya kutatanisha.
Kauli hiyo imetolewa na na Jeshi hilo kutokana na wananchi wa kijiji cha Lugoda kilichopo kata ya Mlondwe kuweka mgomo kuto mzika mkakazi mmoja wa kijiji hicho Bi Salai Nkwama kwa kile kinacho sadikika kuwa mama huyo amefariki kwa imani za kishirikina.
Uchunguzi uliofanywa na madaktari kituo cha afya cha Matamba , imeonekana mama huyo haja fariki kwa imani za kishirikina wanavyo zani wanajamii wa kijiji hicho.
Kwa upande wao wananchi wamesema kifo cha Bi. Salai kimetokea usiku wa kuamkia ambapo mama huyo aliugua ghafla na kukimbizwa kituo cha afya Matamba ambapo alifariki muda mchache baadaye.
Hata hivyo wananchi hao wamesema endapo serikali kutolifumbia macho suala la watu wenye imani za kishirikina kwani kama serikali haitakemea tatizo hilo ndio mwanzo wa uvunjifu wa amani na haki za binadamu.
Hivi karibuni kumekuwa na upigaji kura zoezi liloendelea nchi nzima kuwabaini watu wanaojihusiha na vitendo vya mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi “albino” Habari za uhusika wa ganga wa jadi na imani za kishirikina kwenye mauji hayo zilifichuliwa na mwandihishi mwandamizi wa BBC nchini Bi. Vicky Ntetema.
“Unajua hata vita dhidi ya UKIMWI inakuwa ngumu sana kama tutaendelea kusadiki kuwa watu wanauawa kichawi” alisema Bw. Kambanyuma mwenyekiti wa PIUMA alipokuwa akitafakari pamoja na mwandishi wa habari hii.
