Ujenzi wa Sekondari Iwawa
Na Evance Seth
Wananchi wa kata ya Iwawa wanakabiliwa na shughuli za ujenzi wa majengo yanayoendelea kujengwa shuleni hapo ikiwa pamoja na ujenzi wa Hosteli , Maabara , Maktaba pamoja na jengo kwa ajili ya kidato cha tano na kidato cha sita.
Hayo yamezungumuzwa na Afisa mtendaji wa Kata ya Iwawa Bw Selemani Kiwone katika mazungumzo yake na mwandishi wa habari hii.
Akizungumzia ujenzi huo mkuu wa shule hiyo Bw. Omath Sanga amesema kuwa wananchi wametoa mchango mkubwa katika ujenzi unaoendelea kwa usombaji wa mawe, mbao, uchimbaji kiwanja pamoja na mafundi kujenga majengo hayo.
‘’viongozi wa serikali wanatakiwa kutambua umuhimu kushiriki kikamilifu katika shughuli za ujenzi” alisema Bw. Kiwone. Akifafanua juu ya suala hilo Bw. Kivone alisema katika ujenzi wa shule za ya sekondari baadhi ya viongozi wa Halmashauri wapo nyuma katika kuchangia ujenzi. “Hali hiyo inasababisha kuwakatisha tama wananchi wanaotoa michango pamoja na nguvu zao shuleni hapo” alimalizia Bw. Kiwone.
Naye mkuu wa shule ametoa changamoto zinazo wakabili shuleni hapo kuwa ni pamoja na upungufu wa walimu, nyumba za walimu, baadhi ya vyumba vya madarasa kuto karabatiwa na kusababisha wanafunzi kulundikana katika darasa moja, hali ambayo ina sababisha mwalimu kushindwa kufanya kazi kwa ufanisi.
