Na Witness Ngumba.
Ujenzi wa jengo la PIUMA waenda kasi kwani wanachama wa PIUMA wanapenda ifikapo tarehe 1 December 2009 jengo lao liwelimekwisha na hatimaye waweze kuhamishia ofisi zao zote huko.
Hayo yalisemwa jana na mwenyekiti waPIUMA Bw. Kabuyu Kyando akizungumza na mtandao huu kwenye ofisi ya KatibuTarafa akiwa pamoja na baadhi ya viongozi waPIUMA katika kikao cha pamoja na serikali ya Tarafa.
Mkutano huu ulioitishwa na Katibu tarafa ya Bulongwa Bw. Ambilikile Mwaihola ulikuwa kwa ajili ya kukaa pamoja, kujadilina kupata ufumbuzi juu ya kumaliza jengo la PIUMA haraka.“Nimepata taarifa kuwa pesa za Ujenzi zipo lakini inaonekanakunakosekanauwajibikaji miongoni mwa viongozi na wanachama wa shirika” alisemaKatibu tarafaBw. Mwaihola
Akimtoa wasi wasi katibu tarafa, Mwenyekiti wa PIUMA alisema kuwa yeye na wanachama wa PIUMA wamejipanga kisawa sawa kuhakikisha jengo linaisha ifikapo December mwaka huu. “Mpaka sasa kila siku mwanachama wa PIUMA pamoja na viongozi wana shinda na mafundi kwenye jengo” alisema Bw. Kyando. Aliongeza kuwa kumekuwa na mafundi wakorofi na kuwa fundi ambaye ataonekana anasumbua hatua za kisheria zitachukuliwa juu yake.
Alisema kumekuwa na usumbufu wa hapana pale kutoka kwa mafundi, akitoa mfano Mwenyekiti alisema fundi seremala ameanza kutusumbua tumemwandikia barua ya onyo nakuhakikisha anamaliza kazialiyokuwa amekabidhiwa haraka vinginevyo hatua zakisheriazitachukuliwa.
Veranda imeshaisha kusakafiwa, wiki hili tunategemea kumaliza kufunga milango na hatimaye fundi waumeme na rangi waanze kazi. Tutahakikisha kuwa tunafanya mawasiliano na Mshauriwa wa ujenzi Mtaalam Mwamwala ili awakabidhi kazi mafundi wa umeme na rangi haraka iwezekanavyo. “Nitahakikisha nitalisimamia jengo letu mpaka litakapoisha ili niweze kupata matibabu bora kwa wakati muafaka” alisema Mwenyekiti.
Jengo la PIUMA linatarajiwa kitumika kama kituo cha tiba na ofisi kwa ajili ya upangaji na uendeshaji wa kiliniki ya upimaji na ushauri nasahaa.



