Wednesday, November 18th, 2009

Mradi wa Rafiki wa Vijana

Na Evance Seth

 

Vijana  wa kijiji cha Ivalalila wametakiwa kutumia  HUDUMA  YA RAFIKI KWA VIJANA ili waweze kujitambua.

 

Hayo yamesemwa na  Daktari Bw. Jonathan  Kitundu wakati akitoa elimu  ya Rafiki Kijana iliyo fanyika katika kijiji hicho cha Ivalalila. Daktari Kitundu amesema huduma ya Rafiki inatolewa kwa vijana  ili kukuidhi mahitaji  aliyo nayo kwa muda mwafaka.

 

Amesema vijana wanatakiwa kufika  katika Hospitali, Zahanati, Vituo vya Afya  na vituo vya vijana  kwa ajili ya huduma hiyo  na kuwataka kupima afya zao kwa ajili ya kupanga malengo yao ya baadaye.

 

Na mwisho Katibu wa vijana  tawi  la Ivalalila Bw Agano Sanga  amesema elimu waliyo ipata  itawasaidia vijana kuepukana na  maambukizi ya virusi vya ukimwi hususani katika HUDUMA YA RAFIKI KWA VIJANA.

Leave a Reply