Wednesday, November 18th, 2009

Walemavu na Mikakati

Na Evance Seth

 

Katika wilaya ya Makete kuna kikundi cha walemavu  kilichopo hapahapa Makete kinacho itwa (KICHAWAMA)  kimepanga  mipango madhubuti juu ya kuijengea uwezo  jamii ya watu wenye matatizo  ya ulemavu kwa kutoa elimu ya ufundi stadi pamoja  na kutoa elimu  kwa jamii kutambua  haki za walemavu wa aina zote.

 

Akizungumuza na mwandishi wa habari Mwenyekiti wa kikundi  cha walemavu  Makete Bw. Niko Mbwilo  amesema watu wenye matatizo ya  ulemavu wamefikia hatua  ya kukata tama kutokana na jamii kuona kama  walemavu hawawezi lolote.

 

Bw Mbwilo ameeleza matatizo yanayo wakabili  kuwa ni pamoja na  kukosa nyumba  ya kufundishia  pamoja na  chakula kwa walemavu ambao wangependa  kujifunza fani mbalimbali.

 

Pia amesema  kama kikundi  wameweza kutoa  mafunzo ya ufundi  katika kata ya Ipepo pamoja na kata ya Iwawa, lakini ameomba serikari kuwasaidia kupata idadi ya walemavu  ili kuweza kupanga  miundo mbinu katika mwaka 2010

Leave a Reply