Wanachama wa PIUMA wakifanya usafi kwenye jengo lao.
Na Witness Ngumba
Wanachama wa PIUMA wiki iliyopita walikuwa wanafanya usafi kwenye jengo lao kwa ajili ya maandalizi ya mkutano mkuu wa mwaka.
Akizungumza katibu mkuu Bi. Anna Mwinuka alisema kuwa usafi utafanywa na wanachama walio katika vijiji vya karibu na jengo. Jumla ya wanachama waliofika kwenye usafi walikuwa 17
Usafi uliofanyika ulikuwa ni ndani ya jengo na usafi wa nje ya jengo utafanywa kwa siku nyingine na wanachama wote wa PIUMA baada ya jengo lote kuisha.









