Archive for December, 2009

Monday, December 21st, 2009

Wanachama wa PIUMA wakifanya usafi kwenye jengo lao.

Na Witness Ngumba

 

Wanachama wa PIUMA wiki iliyopita walikuwa wanafanya usafi kwenye jengo lao kwa ajili ya maandalizi ya mkutano mkuu wa mwaka.

 

Akizungumza katibu mkuu Bi. Anna Mwinuka alisema kuwa usafi utafanywa na wanachama walio katika vijiji vya karibu na jengo. Jumla ya wanachama waliofika kwenye usafi walikuwa 17

 

Usafi uliofanyika ulikuwa ni ndani ya jengo na usafi wa nje ya jengo utafanywa kwa siku nyingine na wanachama wote wa PIUMA baada ya jengo lote kuisha.

 

 

 

WanaPIUMA wakifanya usafi

WanaPIUMA wakifanya usafi

Dr. zin zin nae akiwa ndani ya usafi

Dr. zin zin nae akiwa ndani ya usafi

Afisa mtendaji nae akiwa ndani ya kazi

Afisa mtendaji nae akiwa ndani ya kazi

Thursday, December 3rd, 2009

Siku ya UKIMWI duniani 1.12.2009

Na Witness Ngumba

Siku ya UKIMWI duniani ni siku ambayo huwa inaadhimishwa kila mwaka Tanzania nzima kwa ajili ya kuwakumbuka watu waliokufa kwa ugonjwa wa UKIMWI pamoja na wanaoishi na Virusi vya UKIMWI.

 

Kwa Wilaya ya Makete Tarafa  ya Bulongwa Siku hii  imeadhimishwa katika tarafa ya Bulongwa kijiji cha kitula ikiwa ni muunganiko wa kata mbili, kata ya Kipagalo na kata Bulongwa. Sherehe hii ilianza rasmi saa 6:00 mchana ikiongozwa na katibu Tarafa wa Bulongwa Bw. Ambikile Mwaihola, Mgeni rasmi wa sherehe hii alikuwa ni Mh. Diwani Estomih Mahenge. Kauli mbiu ya mwaka huu ilikuwa “UHURU NI UWEZO

 

Mgeni rasmi aliwashukuru watu wote wanaoishi na Virusi vya UKIMWI kwa kufuata taratibu zote za dawa pamoja na mashirika yanayosaidia kutoa huduma ikiwemo PIUMA.

Katika sherehe hii PIUMA waliandaa kwaya, igizo pamoja na kugombea umiss Uhuru Bulongwa, aliyeongoza kwa umiss alikuwa ni Rehema Nyamule, akifuatiwa na  Wema Sanga, Anna Mwinuka,Tulingila Sanga.

Mh. Diwani akitoa zawadi kwa mamiss PIUMA

Mh. Diwani akitoa zawadi kwa mamiss PIUMA

 

 

 Miss uhuru PIUMA 2009 ni Rehema nyamule.

Miss uhuru PIUMA 2009 ni Rehema nyamule.