PIUMA waanza kutembelea vijijini.
Na Witness Ngumba.
Viongozi wa PIUMA pamoja na baadhi ya wanachama wa PIUMA wiki iliyopita walitembelea kijiji cha Utanziwa kwa ajili ya kuwatembelea wanachama wa PIUMA wanaoishi katika kijiji hicho.
Zoezi hili liliongozwa na Katibu Mkuu wa PIUMA pamoja na Mwenyekiti, Daktari Zin zin, na wanachama wawili ambao ni Izack Sanga na John Nyivaha.
Kazi ambazo walikwenda kuzifanya ni pamoja na;
· kuwasajili wanachama waliokuwepo kwa upya kwa kuzingatia vipengele vifuatavyo, kuhakikisha kila mwanachama yumo kwenye orodha ya wanachama hai na waliopiga picha.
· Kutoa ushauri nasaha kwa wasio wanachama ili wajiunge na shirika la PIUMA kwa ajili ya kupata huduma zinazotolewa na shirika.
· Kujua maendeleo ya wanachama kiafya na kwa wale wanaoumwa wapewe huduma inayostahili.
· kwa wale ambao walikuja kwenye zoezi hilo waliombwa kuwaambia wenzao kuwa wafike ofisini ili waweze kupigwa picha kwa ajili ya vitambulisho.
Kwa wale ambao walishindwa kufika kwenye kituo tulichokuwa tumekusanyikia kutokana na afya zao kuwa mbaya tulihakikisha tunawetembelea majumbani kwao ili kuwajulia hali na kuwapa ushauri. Zoezi hili litaendelea kwa kila wiki kwa kijiji kimoja mpaka tutakapomaliza vijiji vyote “alisema Katibu Bi. Anna Mwinuka”








