Archive for January, 2010

Monday, January 25th, 2010

PIUMA waanza kutembelea vijijini.

 

Na Witness Ngumba.

 

Viongozi wa PIUMA pamoja na baadhi ya wanachama wa PIUMA wiki iliyopita walitembelea kijiji cha Utanziwa kwa ajili ya kuwatembelea wanachama wa PIUMA wanaoishi katika kijiji hicho.

 

Zoezi hili liliongozwa na Katibu Mkuu wa PIUMA pamoja na Mwenyekiti,  Daktari Zin zin, na wanachama wawili ambao ni Izack Sanga na John Nyivaha.

 

Kazi ambazo walikwenda kuzifanya ni pamoja na;

·         kuwasajili wanachama waliokuwepo kwa upya kwa kuzingatia vipengele vifuatavyo, kuhakikisha kila mwanachama yumo kwenye orodha ya wanachama hai na waliopiga picha.

·         Kutoa ushauri nasaha kwa wasio wanachama ili wajiunge na shirika la PIUMA kwa ajili ya kupata huduma zinazotolewa na shirika.

·         Kujua maendeleo ya wanachama kiafya na kwa wale wanaoumwa wapewe huduma inayostahili.

·         kwa wale ambao walikuja kwenye zoezi hilo waliombwa kuwaambia wenzao kuwa wafike ofisini ili waweze kupigwa picha kwa ajili ya vitambulisho.

Kwa wale ambao walishindwa kufika kwenye kituo  tulichokuwa tumekusanyikia kutokana na afya zao kuwa mbaya tulihakikisha tunawetembelea majumbani kwao ili kuwajulia hali na kuwapa ushauri. Zoezi hili litaendelea kwa kila wiki kwa kijiji kimoja mpaka tutakapomaliza vijiji vyote “alisema Katibu Bi. Anna Mwinuka”

Timu ya wanaPIUMA wanaotembelea vijijini

Timu ya wanaPIUMA wanaotembelea vijijini

 

 

 

 

 

Wednesday, January 6th, 2010

Mkutano mkuu wa mwaka PIUMA.

Na Witness Ngumba.

Mkutano mkuu wa mwaka wa PIUMA umefanika tarehe 18/12/2009, mgeni rasmi wa mkutano alikuwa ni Mkuu wa Wilaya Bi. Hawa Ng’humbi, wageni wengine waliokuwepo ni pamoja na Joseph Chaula – DAS, Felician Chawala  - Ag. DMO, Hamza – ofisi ya DSO, Erica Sanga – Viti maalumu, Estomih Mahenge – Diwani bulongwa, Ambikile Mwaihola – Afisa Tarafa, Clemence – WEO Bulongwa, Edward Masevela – Ad. BLH, Benitho Ngailo - MASUPHA wanachama wa PIUMA waliokuwa wamehudhuria walikuwa 75  na wengine wengi.

Ilisomwa taarifa ya Katibu na Katibu mkuu pamoja na taarifa ya fedha ilisomwa na Mtunza Hazina wa PIUMA.

Mkuu wa Wilaya alitoa salamu na shukrani nyingi kwa shirika la PIUMA kwa kazi nyingi zinazofanywa na shirika hili hasa  dhidi ya mapambano ya UKIMWI. Aliendelea kusema kuwa alipokuwa alifika katika Wilaya ya Makete shirika ambalo limekuwa likijishughulisha na masuala ya upimaji ni shirika la PIUMA , aliwaasa wanachama wa PIUMA kuendelea kutoa elimu kwa jamii juu ya faida za kupima pamoja na hasara za kutokupima afya zao.

Pamoja na hayo Mkuu wa Wilaya alishukuru kwa ujenzi wa jengo la PIUMA ambalo tunategemea kuwa litakuwa Zahanati ya PIUMA hapo baadaye na kuwaahidi kuwa atachangia kiasi cha sh. 200,000/= kwa ajili ya ujenzi wa jengo la PIUMA.

 

wanachama wa PIUMA wakiwa kwenye mkutano

wanachama wa PIUMA wakiwa kwenye mkutano

 

Mkuu wa Wilaya Bi. Hawa Ng'humbi akitoa hotuba

Mkuu wa Wilaya Bi. Hawa Ng'humbi akitoa hotuba

 

Katibu mkuu akisoma taarifa ya mwaka.

Katibu mkuu akisoma taarifa ya mwaka.

 

Ag. DMO akitoa salamu.

Ag. DMO akitoa salamu.

 

DAS- Makete akitoa salamu

DAS- Makete akitoa salamu