Wednesday, February 17th, 2010

Mtandao wa vijana Makete.

 

Na Evance Seth.

 

Katika Wilaya ya Makete kuna mtandao  mmoja unajishughulisha na vijana unaojulikana kwa jina la MAKEYODEN.

 

Mtandao huo uliamua kufanya kikao cha viongozi wa mtandao tarehe 22/01/2010 na kujadili malengo mbalimbali ya kufanya  2010-2013, na malengo hayo ni kama

 

1.KUBORESHA UONGOZI  ni kufanya marekebisho katiba ya makeyoden, kuandika sera kanuni na taratibu za makeyoden, kanuni za utendaji na uendeshaji , kanuni na taratibu za fedha na kanuni za ustawi na mahusiano na kuendesha vikao vya kamati kuu na mkutano mkuu.

 

2.KUBORESHA UTENDAJI ni kuajili watendaji wa ofisi kuu, kumaliza  ujenzi wa ofisi ya mtandao na vituo vya kata, kununua  samani  na vitendea kazi, kuendesha vikao vya utendaji na  kuanzisha tovuti na internet  ya makeyoden.

 

3.KUBORESHA  MAHUSIANO NA USHIRIKIANO BAINA YA MAKEYODEN NA WADAU WENGINE  ni kuandaa utambulisho wa  shughuli za makeyoden kuandaa orodha ya  wadau mbalimbali, kusambaza utambulisho wa makeyoden kwa njia mbalimbali na kuhudhulia matukio  ya wadau mbalimbali.

 

4.KUENDELEZA SHUGHULI ZA MAKEYODENI ZILIZOPO ni kuhimiza  umaliziaji wa vituo vya kata  tisa , kusaidia vituo saba vilivyokamilika vianze vianze utekelezaji wa mipango na  kukamilisha  usajili wa redio na kutayarisha mpango wa kazi na wa  kujitegemea  wa redio na kuongeza  nguvu  ya kudhibiti maambukizi dhidi ya ukimwi.

 

Kikao hicho kilifanyika  na viongozi wa mtandao  ambao  ni

1.       NAHAMAN SANGA  - MWENYEKITI

2.       JUMA  SINENE  - KATIBU

3.       EMANUEL SANGA  - MWASIBU

4.       FRANCISKO  SIGARA - MJUMBE

5.       SALEHE  NGULO  - MJUMBE

 

Na mwisho viongozi hao walihitimisha kikao  kuagana na kutakiana safari njema.

 

One Response to “Mtandao wa vijana Makete.”


  1. Royal Orr says:

    Hongera sana to the youth of Makete! Perhaps they could work with PIUMA to establish their offices and to afford an Internet connection.

Leave a Reply