Mtandao wa vijana Makete.
Na Evance Seth.
Katika Wilaya ya Makete kuna mtandao mmoja unajishughulisha na vijana unaojulikana kwa jina la MAKEYODEN.
Mtandao huo uliamua kufanya kikao cha viongozi wa mtandao tarehe 22/01/2010 na kujadili malengo mbalimbali ya kufanya 2010-2013, na malengo hayo ni kama
1.KUBORESHA UONGOZI ni kufanya marekebisho katiba ya makeyoden, kuandika sera kanuni na taratibu za makeyoden, kanuni za utendaji na uendeshaji , kanuni na taratibu za fedha na kanuni za ustawi na mahusiano na kuendesha vikao vya kamati kuu na mkutano mkuu.
2.KUBORESHA UTENDAJI ni kuajili watendaji wa ofisi kuu, kumaliza ujenzi wa ofisi ya mtandao na vituo vya kata, kununua samani na vitendea kazi, kuendesha vikao vya utendaji na kuanzisha tovuti na internet ya makeyoden.
3.KUBORESHA MAHUSIANO NA USHIRIKIANO BAINA YA MAKEYODEN NA WADAU WENGINE ni kuandaa utambulisho wa shughuli za makeyoden kuandaa orodha ya wadau mbalimbali, kusambaza utambulisho wa makeyoden kwa njia mbalimbali na kuhudhulia matukio ya wadau mbalimbali.
4.KUENDELEZA SHUGHULI ZA MAKEYODENI ZILIZOPO ni kuhimiza umaliziaji wa vituo vya kata tisa , kusaidia vituo saba vilivyokamilika vianze vianze utekelezaji wa mipango na kukamilisha usajili wa redio na kutayarisha mpango wa kazi na wa kujitegemea wa redio na kuongeza nguvu ya kudhibiti maambukizi dhidi ya ukimwi.
Kikao hicho kilifanyika na viongozi wa mtandao ambao ni
1. NAHAMAN SANGA - MWENYEKITI
2. JUMA SINENE - KATIBU
3. EMANUEL SANGA - MWASIBU
4. FRANCISKO SIGARA - MJUMBE
5. SALEHE NGULO - MJUMBE
Na mwisho viongozi hao walihitimisha kikao kuagana na kutakiana safari njema.

Royal Orr says:
Hongera sana to the youth of Makete! Perhaps they could work with PIUMA to establish their offices and to afford an Internet connection.