Mnada wa Ng’ombe.
Na Evance Seth.
Mnada wa mifugo uliopo katika kijiji cha isapulano kata ya Iwawa ulioanza kujengwa mwaka 2009-2010 kwa ufadhili wa DADS NA DADPS pamoja na nguvu za wananchi ulioghalimu kiasi cha shilingi milioni kumi na nne na thelathini na nane elfu 14,380,000 umezinduliwa .
Uzinduzi wa mnada huo umefanywa na mgeni rasimi ambaye ni mbunge wa wilaya ya makete MH BINILITI SAATANO MAHENGE ambapo amewatakia wananchi wa kijiji cha Isapulano na wananchi wa wilaya makete kwa ujumla kuutumia mnada huo ili kujiongezea kipato.
Aidha ameendelea kusema wananchi wote wanatakiwa kuonesha upendo kwa wageni watokao nje ya makete kwa kuto wakatisha tama kwa kuwaibia mali zao pindi wanapo kuja kwenye mnada huo. Na ameeleza mafanikio yaliyo patikana katika awam ya nne ya uongozi kwa kipindi cha miaka mitatu na nusu kwa wakazi wa wilaya ya makete ambayo ni kufufua zao la pareto pamoja na elimu ambapo kila kata kumejengwa shule za sekondari na wanafunzi wengi kufanikiwa kujiunga na elimu ya sekondari.
Katika sherehe za uzinduzi wa mnada huo MH mahenge aliongozana na mwenyekiti wa Halmashauri wa wilaya ya makete ambaye pia ni diwani wa kata ya Iwawa MH ONO SIKUNALA NKWAMA , mtendaji Iwawa KIWONE , AFISA KILIMO NA MIFUGO WA WILAYA BW ERNEST MKONGO pamoja na watalam wake. Aidha changamoto kubwa inayo ukabili mnada huo ubovu wa barabara inayotoka makete kwenda kijiji hapo ambayo wakati wa masika haipitiki kwa uraisi pamoja na ukosefu wa miundo mbinu ya maji ambapo kwa suala la maji MH ONA nkwama ametoa liri mbili za bomba kwa ajili ya kusogeza maji eneo la mnada na suala barabara kuahidi kushughulikia ipitike muda wote.
Wakiongea kwa nyakati tofauti wananchi wa kijiji hicho wameonekana kufurahishwa na na mnada ambao utakuwa ukifanyika mara mbili kwa mwezi tarehe kumi na tano na tarehe thelathini ya kila mwezi na kusema mifugo yote itauzwa mnadani ili kupata soko la uhakika na si la kuuzia mitaani.
