Monday, February 22nd, 2010

Semina ya usimamizi wa mitihani ya darasa la Saba.

 

Na Evance Seth

 

Semina ya maelekezo  kuhusu  usimamizi wa mtihani  wa taifa  wa kuhitimu elimu ya msingi iliyo fanyika  katika  ukumbi wa Halimashauri ya wilaya ya makete.

 

Akinzungumza katika semina hiyo mkuu wa wilaya ya makete Bi HANA HUMBI  amesema  wasimamizi wanatakiwa  kuepuka vishawishi  kama vile rushwa  katika  zoezi hilo la usimamizi.

Alisema kuwapa watoto mtihani au majibu  ni kujenga  Taifa lenye watu wajinga  wasio na elimu wala  taaluma na kusema  yeyote atakaye gundulika  kufanya hivyo  atawajibika kisheria.

Akifunga semina hiyo Mkurugenzi  wa Halmashauri ya wilaya ya makete  Bi IMELDA ISHUZA  ametaka wasimamizi hao wa mtihani kuwa na upendo  kwa watoto  kwa kuwaelekeza vizuri  pale wanapo hitaji msaada  wa msimamizi.

 

Leave a Reply