Semina ya usimamizi wa mitihani ya darasa la Saba.
Na Evance Seth
Semina ya maelekezo kuhusu usimamizi wa mtihani wa taifa wa kuhitimu elimu ya msingi iliyo fanyika katika ukumbi wa Halimashauri ya wilaya ya makete.
Akinzungumza katika semina hiyo mkuu wa wilaya ya makete Bi HANA HUMBI amesema wasimamizi wanatakiwa kuepuka vishawishi kama vile rushwa katika zoezi hilo la usimamizi.
Alisema kuwapa watoto mtihani au majibu ni kujenga Taifa lenye watu wajinga wasio na elimu wala taaluma na kusema yeyote atakaye gundulika kufanya hivyo atawajibika kisheria.
Akifunga semina hiyo Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya makete Bi IMELDA ISHUZA ametaka wasimamizi hao wa mtihani kuwa na upendo kwa watoto kwa kuwaelekeza vizuri pale wanapo hitaji msaada wa msimamizi.
