Ujenzi wa Zahanati Unyagala.
Na Evance Seth.
Zaidi ya shilingi milioni hamsini na saba pointi nane zinatarajia kutumika kwa ajili ya ujenzi wa zahanati ya Unyangala na Igumbilo katika kipindi cha mwaka 2009-2010 wilayani Makete.
Akizungumza mratibu wa mfuko wa maendeleo ya jamii wilayani Makete Bi Jaklini Mroso ameeleza kuwa fedha hizo zitatumika kwa ajili ya ununuzi wa vifaa vya ujenzi pamoja na nguvu za wananchi zitahitajika kukamilisha miradi hiyo kwa wakati.
Naye katibu wa zahanati ya Unyangala Bw. Boaz Sanga pamoja na mtunza hazina Bw. Erasto Mvela wamesema kuwa msaada huo umekuja kwa wakati kwao kwani wamekuwa wakitumia muda mwingi kuwa peleka wagonjwa katika zahanati ya Utengule ambapo ni mbali.
Mfuko wa maendeleo ya jamii TASAF wilayani Makete umekuwa mkombozi kwa wananchi wengi wilayani Makete hasa vijijini kwa kusaidia misaada mbalimbali ambayo wamekuwa wakiibua kupitia mikutano ya hadhara, aidha kufuatia hali , katibu wa mradi wa ujenzi wa zahanati Igumbilo Bw. Godfrey Sanga ameeleza kuwa zahanati hiyo kwa sasa ipo hatua ya mwisho na ameshukuru TASAF kwa ufaddhili wa mradi huo na amewataka wananchi kuendelea kuunga mkono jitihada zinazo fanywa na TASAF wilayani makete.

Timin Lwilla says:
I have been following with keen interest articles published in your blog.
Big up PIUMA staff and reporters. This really explains the slogan “Makete- wilaya ya kazi”
Timin Lwilla
Lugoda hospital
P O Box 40
MUFINDI