Friday, February 26th, 2010

CHANJO YA WATU WAZIMA

  

Na Evance Seth.

 

Katika Wilaya ya Makete kata ya Iniho  kumefanyika chanjo ya watu wazima  kuanzia miaka mitano na kuendelea.

 

Chanjo hiyo ilikuwa ni agizo la serikari kuwa kila mwananchi anatakiwa kupata  chanjo ilimradi ana miaka kuanzia mitano. Chanjo hiyo  alihudumia  Bw. Tigrath  Sanga toka kata ya Iniho  kwani ndiye  aliye pata mafunzo hayo.

 

Bw. Tigrath kabla ya kuanza kuhudumia alitoa  maelezo kwa ufupi  kwa wananchi wa wake kuwa, chanjo hii ni ya vidonge na alisema  maana ya chanjo hii  ni ya kuzuia magonjwa nyemelezi pamoja na kuua minyoo mwilini, alitoa mfano mmoja wa magonjwa nyemelezi kama  kuvimba matezi.

 

Alisema chanjo hii hawaruhusiwi  watoto wadogo kupata  kwani vidonge hivi vina nguvu sana mwilini vinapo fanya kazi , na alisema upatapo chanjo hii huruhusiwi kutumia kinywaji cha aina ya kileo  kwa siku  uliyopata chanjo.

 

 

 

Leave a Reply