CHANJO YA WATU WAZIMA
Na Evance Seth.
Katika Wilaya ya Makete kata ya Iniho kumefanyika chanjo ya watu wazima kuanzia miaka mitano na kuendelea.
Chanjo hiyo ilikuwa ni agizo la serikari kuwa kila mwananchi anatakiwa kupata chanjo ilimradi ana miaka kuanzia mitano. Chanjo hiyo alihudumia Bw. Tigrath Sanga toka kata ya Iniho kwani ndiye aliye pata mafunzo hayo.
Bw. Tigrath kabla ya kuanza kuhudumia alitoa maelezo kwa ufupi kwa wananchi wa wake kuwa, chanjo hii ni ya vidonge na alisema maana ya chanjo hii ni ya kuzuia magonjwa nyemelezi pamoja na kuua minyoo mwilini, alitoa mfano mmoja wa magonjwa nyemelezi kama kuvimba matezi.
Alisema chanjo hii hawaruhusiwi watoto wadogo kupata kwani vidonge hivi vina nguvu sana mwilini vinapo fanya kazi , na alisema upatapo chanjo hii huruhusiwi kutumia kinywaji cha aina ya kileo kwa siku uliyopata chanjo.
