Sensa ya Mifugo.
Na Evance Seth.
Makarani na wasimamizi wa SENSA ya mifugo wamepatiwa mafunzo yatakayo wawezesha kupima mpango mzima wa kuondoa kwenye sekta ya kilimo na mifugo kwa mwaka 2009/2010.
Akifungua mafunzo hayo yaliyofanyika katika wilaya ya Makete kaimu katibu tawala wa mkoa wa Iringa Bw. Adam Swai amesema mwaka 2008 mpango wa sekta ya kilimo kwa pato la taifa kulikuwa ni asilimia 25.8, kati ya asilimia hiyo ya kilimo cha mazao kilichangia asilimia 19 huku mifugo ikichangia asilimia 4.7.
Kwa upande Meneja takwimu mkoa wa Iringa amesema sense hiyo hufanyika kila baada ya miaka mitano na kwamba katika mafunzo hayo watachagua wakulima kumi , kutoka katika mafunzo hayo watachagua wakulima kumi na tano kutokana na vigezo vilivyowekwa vya wakulima bora katika kila wilaya .
