Friday, February 26th, 2010

Sensa ya Mifugo.

Na Evance Seth.

Makarani na  wasimamizi  wa SENSA  ya mifugo  wamepatiwa mafunzo yatakayo wawezesha  kupima mpango mzima  wa kuondoa  kwenye sekta ya kilimo na mifugo  kwa mwaka 2009/2010.

 

Akifungua mafunzo hayo  yaliyofanyika katika  wilaya ya Makete  kaimu katibu tawala wa mkoa  wa Iringa  Bw. Adam Swai amesema  mwaka 2008  mpango wa sekta ya kilimo kwa pato la taifa  kulikuwa ni asilimia  25.8, kati ya asilimia hiyo ya kilimo  cha mazao  kilichangia  asilimia 19 huku mifugo  ikichangia asilimia 4.7.

 

Kwa upande Meneja takwimu  mkoa wa Iringa  amesema  sense  hiyo hufanyika  kila baada ya miaka mitano na kwamba  katika mafunzo  hayo  watachagua  wakulima kumi , kutoka  katika  mafunzo hayo watachagua  wakulima kumi na tano kutokana na vigezo vilivyowekwa  vya wakulima bora  katika kila wilaya .

Leave a Reply