Watumishi wa UMA
Na Evance Seth.
Ofisi ya Rais menejimenti ya utumishi wa UMA inakusudia kuwa watumishi wa serikari kuanza kupokea mishahara dirishani badara ya kuwaingizia katika akaunti zao.
Kauli hiyo imetolewa na waziri wa Nchi ofisi ya Rais menejimenti ya utumishi wa uma Mh. Hawa Ghasia alipokuwa akiwahutubia watumishi wa halmashauri ya wilaya ya makete. Alisema ofisi yake inafikilia kufanya hivyo kutokana na kulipa mishara hewa ya watumishi.
Mpango huo wa watumishi kupokea dirishani utasaidia kuondoa udanganyifu ambao serikari inalipa mishahara hewa na kusababisha serikari hasara kubwa. Amesema katika kupitia utafiti uliofanywa na wizara yake imebaini katika sekta ya afya na sekta ya elimu baadhi ya watumishi wanalipwa mishahara hewa.
Mh. Ghasia alikuwa katika ziara yake ya kutoa semina kwa halmashauri ya wilaya ya makete inyohusu mabadiliko mahali pa kazi na utawala bora ambapo hii leo akitoka hapa anaelekea wilayani Ludewa.
Mikoa mingine ambayo amepitia kutoa semina hiyo ni MANYARA, KIGOMA, LINDI, MTWARA, PWANI , IRINGA na akimalizia SINGIDA.

joseph says:
Jamani yaani tumeshindwa kabisa kutumia kumbukumbu zinazokusanywa kila mwaka kwa kujua ni nani yupo kazini na nani hayupo kazini ili kuondoa watumishi hewa na badala yake tunarudi tena kule mwaka arobaini na saba kwenye tatizo la mishahara kucheleweshwa na kuongeza wimbi la ujambazi kwenye swala zima la mishahara ya watumishi.
Kweli safari ni ndefu kwenye swala la technolojia na kuna kazi kwenye hii nchi bila mabadiliko ya kweli safari bado ni ndefu sana wandugu.