Na Evance Seth
Katika uwanja wa Luvanyina uliopo kata ya Bulongwa , kumefanyika mechi ya kirafiki ya mpira wa miguu kati ya shule ya sekondari ya mwakavuta na shule ya sekondari kipagalo.
Kwani shule hizo zimekutana ikiwa mwakavuta sekondari ni kongwe ilianza mwaka 1992 na Kipagalo ilanza mwaka 2007.
Mchezo huo ulianza mnamo muda wa saa kumi kamili alasili na mchezo huo uliendeshwa na refarii Bw Timu Sanga. Mnamo dakika ya kumi na mbili Kipagalo walianza kuandika goli la kwanza kupitia kwa mchezaji wao Noah Sanga huku Mwakavuta wakiwa hawajapata kitu, mpira uliendelea huku mwakavuta wakiendelea kushambuliwa na dakika ya thelathini na saba Kipagalo walifunga goli la pili kupitia kwa mshambuliaji wao Juma Nsemwa , hadi mpira unakwenda mapumziko Kipagalo mbili na Mwakavuta sifuri.
Kipindi cha pili kilianza kwa nguvu sana pande zote mbili, huku Mwakavuta Sekondari wakishambulia kwa nguvu sana goli la Kipagalo na dakika ya hamsini na nne mwakavuta wafunga goli la kwanza kupitia kwa mchezaji wao Partson Mbogela na dakika ya sitini na tisa Mwakavuta walifunga goli la pili kupitia kwa mchezaji wao Frank Fungo lililo fungwa kwa njia ya faulo , na Mwakavuta walizidi kuliandama goli la Kipagalo huku kipagalo wakizidi kuchoka , mnamo dakika ya themanini na tatu mwakavuta walifunga goli la tatu kupitia kwa mchezaji wao Regi Sanga na dakika ya tisini na mbili za nyongeza mwakavuta walifunga goli la nne kupitia kwa mchezaji wao yuleyule Frank Fungo hadi mpira unamalizika Mwakavuta Sekondari nne na Kipagalo Sekondari mbili.
Mwalimu wa michezo wa shule ya Sekondari ya Kipagalo alisema kwamba nimekubali matokeo kwani mpira wa miguu una matokeo ya aina tatu kufunga , kufungwa na kutoa sale , naye mwalimu wa Mwakavuta sekondari alisema kwamba nimefurahi sana na ushindi kwani kipindi cha kwanza tulitangulizwa goli mbili bila nilipata tabu kwani kwa sasa nina jiandaa wiki ijayo kuwapeleka vijana wangu kucheza na shule ya Sekondari Ipelele.