Wednesday, March 31st, 2010

Maisha katika kipindi cha mtazamo.

Na Evance Seth.

Imefahamika  kuto jipenda  kwa baadhi ya akina  mama na kutokuwa na  ubunifu  wa miradi ndio  sababisho  kubwa  kuwafanya wanaume  kuleta visa  katika ndoa zao.

Wakichangia   dondoo  za maisha  katika kipindi  cha mtazamo  cha Kitulo FM Redio  , baadhi ya wachangiaji  hao wamesema  matatizo hayo katika ndoa  yanasababishwa na wanawake wenyewe kwa kukosa ubunifu katika  ndoa zao.

Aidha wamesema  wakati mwingine  baadhi ya wanawake  hujisahau mara wanapokuwa  ndani  ya ndoa zao  pamoja na kuacha  kuboresha usafi katika familia zao. Pia imeonekana  baadhi ya akina baba  wamekosa elimu ya ndoa  pamoja na uvumilivu.

Kipindi cha mtanzamo hurushwa kila jumatatu na ijumaa  kuanzia saa tatu kamili asubuhi  mpaka  saa saba kamili mchana  katika  studio za KITULO FM RADIO.

Leave a Reply