Wednesday, March 31st, 2010

Matokeo ya kidato cha Nne.

 Na Evance Seth.

Kumetokea mabadiliko  katika kiwango cha kufaulu kwa wanafunzi  tofauti na mwaka  uliopita  katika shule ya sekondari  Iwawa iliyopo wilayani Makete.

 Akizungumuza  mkuu wa  shule hiyo  Bw OMATH SANGA  amesema jumla ya  wanafunzi mia moja kumi na nane waliofanya mtihani wa Taifa,  wanafunzi wawili wamepata  divisheni one , wanafunzi  kumi na tatu wamepata divisheni two  na wanafunzi thelathini na saba wamepata divisheni three, wakati wanafunzi wane wamepata divisheni ziro.

Mwalimu OMATH SANGA  amesema mpaka sasa  hajapata tathimini  ya kujua  shule yake  imepanda kiasi gani  au imeshuka  kiasi gani  kulingana na shule zingine ,na  hivyo mwisho  amewaomba wananchi  kutambua  umuhimu wa kuwatafutia nafasi za masomo watoto wao.

 

Leave a Reply