Wednesday, March 31st, 2010

Mvua za ezua Mapaa.

Na Evance Seth.

 

Katika wilaya ya makete  Tarafa ya Bulongwa na Magoma kata ya Ipelele na kata ya Kipagalo kumetokea na hasara kubwa itokanayo na mvua.

 

Viongozi wa tarafa  zote mbili wakimweleza  mwenyekiti wa Halmashauri wa wilaya ya makete Mh Ona Skunara Nkwama walisema wiki hii mvua  kubwa sana  imenyesha ikiambatana na upepo mkali imesababisha maafa ya nyumba za wananchi pamoja na shule moja ya msingi  kuezuriwa.

 

Mwenyekiti wa halmashauri  wa wilaya wa makete  alifika sehemu zote za matukio na kutoa pole kwa wananchi wa tarafa zote mbili  na kuahidi kutoa mchango  wa bati kila nyumba .

 

Na wananchi   walimshukuru mwenyekiti wa halmashauri na kusema  tunamshukuru mungu kwani hakuna aliyepata jeraha wala kufa. Na mwisho  mwenyekiti huyo aliwaambia wananchi hao kuwa  mvua zinapo nyesha wazazi tujitahidi kuwa nyumbani kwenye familia zetu kwa ajili ya msaada endapo linatokea swala kama hili kwani mvua bado zinaendelea kunyesha.

 

 

 

 

 

Leave a Reply