Shamba la Ng’ombe Kitulo.
Na Evance Seth.
Akisoma taarifa ya shamba hilo kwa mkuu wa mkoa wa Iringa MH MOHAMEDI ABDILAZIZI mwakilishi wa shamba hilo amesema lengo la shamba hilo ni kuongeza ng’ombe wazalishaji pamoja na kufufua zaidi ya hekta hamsini za malisho kwa kutoa magugu na kuweka mbolea.
Amesema kwa kufanya hivyo utaboresha uzalishaji mkubwa wa kiwanda hicho kwa upande wa ulaji wa ng’ombe wenye afya na uzito wa kutosha punde unapofika wakati wa kuuzwa. Amesema mbali na hatua hiyo pia shamba lina mpango wa kuongeza ng’ombe katika kundi la ukamilishaji kufikia ng’ombe mia mbili ili kupata ndama bora kwa ajili ya kusambaza kwa wakulima.
Malengo mengine ni kuboresha upatikanaji wa maji hasa wakati wa kiangazi pamoja na kutengeneza njia za ndani ya shamba hili zipitike wakati wote na kumalisha ukarabati wa nyumba za watumishi pamoja na kuendelea kuingiza umeme kwenye nyumba za watumishi.

Danny Tweve says:
Thanks for introducing this blog, I will be a part of contributers of this blog
thanks again
Danny Tweve
Mwana Makete
Environmental Planner
0764947555
Royal Orr says:
Thanks, Danny!