Wednesday, March 31st, 2010

Shamba la Ng’ombe Kitulo.

Na Evance Seth.

Akisoma taarifa ya shamba hilo kwa mkuu wa mkoa wa Iringa  MH MOHAMEDI ABDILAZIZI  mwakilishi wa  shamba hilo  amesema lengo la shamba hilo  ni kuongeza ng’ombe wazalishaji  pamoja na kufufua zaidi  ya hekta hamsini  za malisho kwa kutoa  magugu na kuweka mbolea.

Amesema kwa kufanya hivyo  utaboresha  uzalishaji mkubwa wa kiwanda  hicho kwa upande  wa ulaji wa ng’ombe  wenye afya na uzito  wa kutosha punde  unapofika wakati wa kuuzwa. Amesema mbali na  hatua hiyo  pia shamba lina mpango  wa kuongeza   ng’ombe  katika kundi la ukamilishaji kufikia ng’ombe  mia mbili ili kupata ndama bora  kwa ajili ya kusambaza kwa wakulima.

Malengo mengine ni  kuboresha upatikanaji wa maji hasa wakati wa kiangazi  pamoja na kutengeneza njia za ndani ya shamba hili  zipitike wakati wote  na kumalisha  ukarabati wa nyumba za watumishi pamoja na kuendelea  kuingiza umeme kwenye nyumba za watumishi.

2 Responses to “Shamba la Ng’ombe Kitulo.”


  1. Danny Tweve says:

    Thanks for introducing this blog, I will be a part of contributers of this blog
    thanks again
    Danny Tweve
    Mwana Makete
    Environmental Planner
    0764947555


  2. Royal Orr says:

    Thanks, Danny!

Leave a Reply