Wednesday, March 31st, 2010

Uogeshaji wa Ng’ombe.

 

Na Evance Seth

 

Katika kata ya Iniho wamejipatia Josho  kwa ajili ya kuogeshea ng’ombe. Afisa mifugo wa kata ya hiyo  Bw. Nova  alisema kwamba  tumepata josho hili kwa malengo ya kuogeshea ng’ombe  ili kuua wadudu kama kupe na nk.

 

Pia alisema josho hili  ni letu sisi wenyewe kinachotakiwa  kila mwananchi mwenye ng’ombe  anapokuja kuogesha  atalipia shilinngi mia moja kwa kila ng’ombe na hizo fedha zitafanya kazi ya kutengenezea josho pale linapo halibika na kununulia dawa za kuogeshea ng’ombe.

 

Na mwisho alisema kuwa itapangwa ratiba ya kuogesha ng’ombe kwa vijiji  kwani kwa mwezi ni mara moja na kwa yule ambaye ataonekana ajaogesha ng’ombe atachukuliwa hatua ya kisheria

 

Leave a Reply