Uogeshaji wa Ng’ombe.
Na Evance Seth
Katika kata ya Iniho wamejipatia Josho kwa ajili ya kuogeshea ng’ombe. Afisa mifugo wa kata ya hiyo Bw. Nova alisema kwamba tumepata josho hili kwa malengo ya kuogeshea ng’ombe ili kuua wadudu kama kupe na nk.
Pia alisema josho hili ni letu sisi wenyewe kinachotakiwa kila mwananchi mwenye ng’ombe anapokuja kuogesha atalipia shilinngi mia moja kwa kila ng’ombe na hizo fedha zitafanya kazi ya kutengenezea josho pale linapo halibika na kununulia dawa za kuogeshea ng’ombe.
Na mwisho alisema kuwa itapangwa ratiba ya kuogesha ng’ombe kwa vijiji kwani kwa mwezi ni mara moja na kwa yule ambaye ataonekana ajaogesha ng’ombe atachukuliwa hatua ya kisheria
