Archive for the ‘News’ Category

Saturday, May 29th, 2010

Who killed Veneranda?

By Pamoja

Who killed Veneranda? (To watch a video click on the link)

 

Veneranda, who died at the age of 17, stands as a symbol of all People Living with HIV/AIDS (PLWHA) in Bulongwa/ Makete District/ Tanzania, who were denied state-of-the-art treatment due to the misuse and theft of funds designated for their health care.

 

The documentary is dedicated to the 70 HIV-patients – many of them activists from the HIV/AIDS self-help group PIUMA (piuma-simba.org) – who died unnecessarily since 2006 due to the lack of decent HIV-care.

 

If you want to know more about Veneranda and PIUMA, read the article “Veneranda: Struggle of an AIDS-infected orphan” written by the award winning Tanzanian journalist Vicky Ntetema, former bureau chief of the BBC Tanzania, under the following link: pamoja.at/Press_Archives/Veneranda_Struggle_of_an_AIDS-infected_orphan.pdf 

Support combating fatal corruption and donate via credit card, PayPal or transfer your donation directly to our account: pamoja.at/support_us.html

You’ll also find more information in our press archives (pamoja.at/press.html) and on our Facebook pages:

facebook.com/home.php?#!/pages/Who-Killed-Veneranda/111468755554168?v=wall&ref=sgm

_ _

This documentary is dedicated to the 70 HIV-patients – many of them activists from the HIV/AIDS self-help group PIUMA – who died unnecessarily since 2006 due to the lack of decent HIV-care. They did not die from AIDS, but from corruption and disrespect for the human rights to life and treatment. “Veneranda: Struggle of an AIDS-infected orphan” written by the award winning journalist Vicky Ntetema, former BBC bureau chief for Tanzania, or search our press archives  
PAMOJA - TOGETHER - Association for Intl. Cooperation owns the copyrights for the documentary “Who killed Veneranda?”. Feel free to download, upload and distribute the file for non-commercial use!
Source:http://www.pamoja.at/videos.html
Wednesday, March 31st, 2010

Matokeo ya kidato cha Nne.

 Na Evance Seth.

Kumetokea mabadiliko  katika kiwango cha kufaulu kwa wanafunzi  tofauti na mwaka  uliopita  katika shule ya sekondari  Iwawa iliyopo wilayani Makete.

 Akizungumuza  mkuu wa  shule hiyo  Bw OMATH SANGA  amesema jumla ya  wanafunzi mia moja kumi na nane waliofanya mtihani wa Taifa,  wanafunzi wawili wamepata  divisheni one , wanafunzi  kumi na tatu wamepata divisheni two  na wanafunzi thelathini na saba wamepata divisheni three, wakati wanafunzi wane wamepata divisheni ziro.

Mwalimu OMATH SANGA  amesema mpaka sasa  hajapata tathimini  ya kujua  shule yake  imepanda kiasi gani  au imeshuka  kiasi gani  kulingana na shule zingine ,na  hivyo mwisho  amewaomba wananchi  kutambua  umuhimu wa kuwatafutia nafasi za masomo watoto wao.

 

Wednesday, March 31st, 2010

Michezo

Na Evance Seth

Katika  uwanja wa Luvanyina uliopo kata ya Bulongwa , kumefanyika mechi ya kirafiki  ya mpira wa miguu kati ya shule ya sekondari ya mwakavuta na shule ya sekondari kipagalo.

Kwani  shule hizo zimekutana  ikiwa mwakavuta sekondari ni kongwe  ilianza mwaka 1992 na  Kipagalo ilanza mwaka 2007.

Mchezo huo ulianza  mnamo muda wa saa kumi kamili alasili na mchezo huo uliendeshwa na refarii Bw Timu Sanga. Mnamo dakika ya kumi na mbili  Kipagalo walianza kuandika goli la kwanza kupitia kwa mchezaji wao Noah Sanga huku Mwakavuta wakiwa hawajapata kitu, mpira uliendelea  huku mwakavuta  wakiendelea kushambuliwa  na dakika ya  thelathini na saba  Kipagalo walifunga goli la pili kupitia kwa mshambuliaji wao Juma Nsemwa , hadi mpira unakwenda mapumziko  Kipagalo mbili na Mwakavuta  sifuri.

Kipindi cha pili kilianza kwa nguvu sana pande zote mbili,  huku Mwakavuta  Sekondari  wakishambulia kwa nguvu sana goli la Kipagalo  na dakika ya  hamsini na nne mwakavuta wafunga goli la kwanza kupitia kwa mchezaji wao Partson Mbogela na dakika  ya sitini na tisa  Mwakavuta walifunga goli la pili kupitia kwa mchezaji wao Frank Fungo lililo fungwa kwa njia ya faulo , na Mwakavuta walizidi kuliandama goli la Kipagalo  huku kipagalo wakizidi kuchoka  , mnamo dakika ya  themanini na tatu mwakavuta walifunga goli la tatu kupitia kwa mchezaji wao Regi Sanga  na dakika ya tisini na mbili za nyongeza  mwakavuta walifunga goli la nne kupitia kwa mchezaji wao  yuleyule  Frank Fungo   hadi mpira unamalizika  Mwakavuta Sekondari nne na Kipagalo Sekondari mbili.

Mwalimu wa  michezo wa shule ya Sekondari ya Kipagalo  alisema  kwamba  nimekubali matokeo  kwani mpira wa miguu una matokeo ya aina tatu  kufunga , kufungwa na kutoa sale , naye mwalimu wa Mwakavuta  sekondari alisema kwamba nimefurahi sana na ushindi  kwani kipindi cha kwanza tulitangulizwa goli mbili bila  nilipata tabu kwani kwa sasa nina jiandaa  wiki ijayo  kuwapeleka  vijana  wangu  kucheza na shule ya Sekondari Ipelele.

 

Wednesday, March 31st, 2010

Shamba la Ng’ombe Kitulo.

Na Evance Seth.

Akisoma taarifa ya shamba hilo kwa mkuu wa mkoa wa Iringa  MH MOHAMEDI ABDILAZIZI  mwakilishi wa  shamba hilo  amesema lengo la shamba hilo  ni kuongeza ng’ombe wazalishaji  pamoja na kufufua zaidi  ya hekta hamsini  za malisho kwa kutoa  magugu na kuweka mbolea.

Amesema kwa kufanya hivyo  utaboresha  uzalishaji mkubwa wa kiwanda  hicho kwa upande  wa ulaji wa ng’ombe  wenye afya na uzito  wa kutosha punde  unapofika wakati wa kuuzwa. Amesema mbali na  hatua hiyo  pia shamba lina mpango  wa kuongeza   ng’ombe  katika kundi la ukamilishaji kufikia ng’ombe  mia mbili ili kupata ndama bora  kwa ajili ya kusambaza kwa wakulima.

Malengo mengine ni  kuboresha upatikanaji wa maji hasa wakati wa kiangazi  pamoja na kutengeneza njia za ndani ya shamba hili  zipitike wakati wote  na kumalisha  ukarabati wa nyumba za watumishi pamoja na kuendelea  kuingiza umeme kwenye nyumba za watumishi.

Wednesday, March 31st, 2010

Mvua za ezua Mapaa.

Na Evance Seth.

 

Katika wilaya ya makete  Tarafa ya Bulongwa na Magoma kata ya Ipelele na kata ya Kipagalo kumetokea na hasara kubwa itokanayo na mvua.

 

Viongozi wa tarafa  zote mbili wakimweleza  mwenyekiti wa Halmashauri wa wilaya ya makete Mh Ona Skunara Nkwama walisema wiki hii mvua  kubwa sana  imenyesha ikiambatana na upepo mkali imesababisha maafa ya nyumba za wananchi pamoja na shule moja ya msingi  kuezuriwa.

 

Mwenyekiti wa halmashauri  wa wilaya wa makete  alifika sehemu zote za matukio na kutoa pole kwa wananchi wa tarafa zote mbili  na kuahidi kutoa mchango  wa bati kila nyumba .

 

Na wananchi   walimshukuru mwenyekiti wa halmashauri na kusema  tunamshukuru mungu kwani hakuna aliyepata jeraha wala kufa. Na mwisho  mwenyekiti huyo aliwaambia wananchi hao kuwa  mvua zinapo nyesha wazazi tujitahidi kuwa nyumbani kwenye familia zetu kwa ajili ya msaada endapo linatokea swala kama hili kwani mvua bado zinaendelea kunyesha.

 

 

 

 

 

Wednesday, March 31st, 2010

Maisha katika kipindi cha mtazamo.

Na Evance Seth.

Imefahamika  kuto jipenda  kwa baadhi ya akina  mama na kutokuwa na  ubunifu  wa miradi ndio  sababisho  kubwa  kuwafanya wanaume  kuleta visa  katika ndoa zao.

Wakichangia   dondoo  za maisha  katika kipindi  cha mtazamo  cha Kitulo FM Redio  , baadhi ya wachangiaji  hao wamesema  matatizo hayo katika ndoa  yanasababishwa na wanawake wenyewe kwa kukosa ubunifu katika  ndoa zao.

Aidha wamesema  wakati mwingine  baadhi ya wanawake  hujisahau mara wanapokuwa  ndani  ya ndoa zao  pamoja na kuacha  kuboresha usafi katika familia zao. Pia imeonekana  baadhi ya akina baba  wamekosa elimu ya ndoa  pamoja na uvumilivu.

Kipindi cha mtanzamo hurushwa kila jumatatu na ijumaa  kuanzia saa tatu kamili asubuhi  mpaka  saa saba kamili mchana  katika  studio za KITULO FM RADIO.

Wednesday, March 31st, 2010

Uogeshaji wa Ng’ombe.

 

Na Evance Seth

 

Katika kata ya Iniho wamejipatia Josho  kwa ajili ya kuogeshea ng’ombe. Afisa mifugo wa kata ya hiyo  Bw. Nova  alisema kwamba  tumepata josho hili kwa malengo ya kuogeshea ng’ombe  ili kuua wadudu kama kupe na nk.

 

Pia alisema josho hili  ni letu sisi wenyewe kinachotakiwa  kila mwananchi mwenye ng’ombe  anapokuja kuogesha  atalipia shilinngi mia moja kwa kila ng’ombe na hizo fedha zitafanya kazi ya kutengenezea josho pale linapo halibika na kununulia dawa za kuogeshea ng’ombe.

 

Na mwisho alisema kuwa itapangwa ratiba ya kuogesha ng’ombe kwa vijiji  kwani kwa mwezi ni mara moja na kwa yule ambaye ataonekana ajaogesha ng’ombe atachukuliwa hatua ya kisheria

 

Friday, February 26th, 2010

Sensa ya Mifugo.

Na Evance Seth.

Makarani na  wasimamizi  wa SENSA  ya mifugo  wamepatiwa mafunzo yatakayo wawezesha  kupima mpango mzima  wa kuondoa  kwenye sekta ya kilimo na mifugo  kwa mwaka 2009/2010.

 

Akifungua mafunzo hayo  yaliyofanyika katika  wilaya ya Makete  kaimu katibu tawala wa mkoa  wa Iringa  Bw. Adam Swai amesema  mwaka 2008  mpango wa sekta ya kilimo kwa pato la taifa  kulikuwa ni asilimia  25.8, kati ya asilimia hiyo ya kilimo  cha mazao  kilichangia  asilimia 19 huku mifugo  ikichangia asilimia 4.7.

 

Kwa upande Meneja takwimu  mkoa wa Iringa  amesema  sense  hiyo hufanyika  kila baada ya miaka mitano na kwamba  katika mafunzo  hayo  watachagua  wakulima kumi , kutoka  katika  mafunzo hayo watachagua  wakulima kumi na tano kutokana na vigezo vilivyowekwa  vya wakulima bora  katika kila wilaya .

Friday, February 26th, 2010

Watumishi wa UMA

 

Na Evance Seth.

 

Ofisi ya Rais  menejimenti ya utumishi wa UMA inakusudia kuwa watumishi  wa serikari  kuanza  kupokea mishahara  dirishani  badara ya kuwaingizia  katika akaunti zao.

Kauli hiyo imetolewa  na waziri wa  Nchi  ofisi ya Rais  menejimenti ya utumishi wa uma Mh. Hawa Ghasia alipokuwa akiwahutubia watumishi  wa halmashauri ya wilaya ya makete. Alisema  ofisi yake inafikilia  kufanya hivyo kutokana na  kulipa mishara hewa ya watumishi.

 

Mpango huo  wa watumishi kupokea dirishani  utasaidia kuondoa udanganyifu ambao serikari inalipa mishahara hewa na kusababisha  serikari hasara kubwa. Amesema katika kupitia  utafiti  uliofanywa na wizara yake imebaini katika sekta  ya afya  na sekta ya elimu  baadhi ya watumishi  wanalipwa  mishahara hewa.

Mh. Ghasia  alikuwa  katika ziara yake ya  kutoa semina  kwa halmashauri ya wilaya ya makete inyohusu mabadiliko  mahali pa kazi  na utawala bora  ambapo hii leo  akitoka hapa anaelekea  wilayani Ludewa.

Mikoa mingine ambayo amepitia  kutoa semina hiyo ni  MANYARA, KIGOMA, LINDI, MTWARA, PWANI , IRINGA  na akimalizia SINGIDA.

Friday, February 26th, 2010

CHANJO YA WATU WAZIMA

  

Na Evance Seth.

 

Katika Wilaya ya Makete kata ya Iniho  kumefanyika chanjo ya watu wazima  kuanzia miaka mitano na kuendelea.

 

Chanjo hiyo ilikuwa ni agizo la serikari kuwa kila mwananchi anatakiwa kupata  chanjo ilimradi ana miaka kuanzia mitano. Chanjo hiyo  alihudumia  Bw. Tigrath  Sanga toka kata ya Iniho  kwani ndiye  aliye pata mafunzo hayo.

 

Bw. Tigrath kabla ya kuanza kuhudumia alitoa  maelezo kwa ufupi  kwa wananchi wa wake kuwa, chanjo hii ni ya vidonge na alisema  maana ya chanjo hii  ni ya kuzuia magonjwa nyemelezi pamoja na kuua minyoo mwilini, alitoa mfano mmoja wa magonjwa nyemelezi kama  kuvimba matezi.

 

Alisema chanjo hii hawaruhusiwi  watoto wadogo kupata  kwani vidonge hivi vina nguvu sana mwilini vinapo fanya kazi , na alisema upatapo chanjo hii huruhusiwi kutumia kinywaji cha aina ya kileo  kwa siku  uliyopata chanjo.