Archive for the ‘News’ Category

Friday, October 23rd, 2009

Matumizi ya Benki Yaongezeka Makete

Na Evance Seth

 

Meneja wa NMB tawi la Makete Bi. Doris  Luvanda amesema kumekuwa na ongezeko kubwa la wateja wa Benki hiyo katika msimu wa Januar hadi machi kwa mwaka huu 2009.

 

Bi. Luvanda ameyasema hayo wiki iliyopita alipokuwa akizungumza na na mwandishi wa habari hizi kuhusu hali ya ongezeko la wateja pamoja na huduma na huduma zitolewazo na Benki ya NMB tawi la Makete.

 

Aidha amesema kuwa wateja wote waliokuwa wamejaza fomu kwa ajili ya kupata kadi za ATM, kadi zao zimekwisha wasili tangu mwezi wa pili mwaka huu. Hata hivyo Bi. Luvanda alitoa angalizo kw wateja watakao chelewakuchukua kadi zao, “atakayechelewa kuchukua kadi hizo ndani ya miezi sita atatakiwa kuomba upya na atalazimikakulipia gharama za kadi upya yaani kamisheni” aliongeza Bi. Luvanda.

 

Akielezea hali ya watu waliofariki wakati wakiendesha akaunti zao katika Benki hiyo amewaomba ndugu wa marehemu kufika katika benki hiyo ili kupata maelezo ya kina na namna ya kupata pesa katika akaunti za marehemu hao.

 

Bi. Luvanda amewataka wale wote waliofungua akaunti katika benki hiyo na kukaa zaidi ya mwaka mmoja bila bila kuweka wala kuchukua fedha, hivyo kusababisha akaunti zao kulala wanatakiwa kufika na picha za paspoti size ili kufufua akaunti zao.

 

Kumekuwa na ongezeko kubwa la utunzaji wa pesa kwa wanachi wa Makete hivi karibu, Vijana wengi wamekuwa wakitunza pesa zao benki.

Friday, October 23rd, 2009

Vijana Makete Kusoma Ufundi

Na Evance Seth

 

Mkurugenzi mkuu wa VETA nchini Bwana. Zebadia Moshi akiwa ameongozana na baadhi ya wakurugenzi wa VETA nchini mwezi uliopita walikabidhiwa rasmi na uongozi wa Halmashauri ya Wilaya Makete mkataba wa kuanza kujengwa kwa chuo cha VETA wilayani Makete.

 

Akizungumza na Kitulo FM mwezi uliopita Bw. Moshi alisema kuwa mpango wa serikali ni kujenga vyuo 126 kwa awamu tatu katika wilaya zote hapa nchini, ambapo awamu ya kwanza vitajengwa vyuo thelathini, na Wilaya ya Makete ikiwa imepewa nafasi ya kwanza Kitaifa kuanza ujenzi wa chuo cha VETA.

 

Aidha  ameishukuru Halmashauri ya Wilaya ya Makete kwa utekelezaji wa kutafuta hatimiliki pamoja na maandalizi ya miundo mbinu ya mahali kitakapojengwa chuo hicho.

 

Naye Mkuu wa Wilaya ya Makete Bi. Hawa Humbi na mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya Mh. Ona Amosi  Sikunala Nkwama amesema kuwa kujengwa kwa chuo hicho kutasaidia vijana wa Makete kupata elimu ya ufundi kwani mbao zinazouzwa nje ya wilaya zitaboreshwa kwa kutengeneza vifaa bora vitakavyouzwa ndani na nje ya Wilaya.

 

Jumla ya shilingi Bilioni tatu zimetengwa kwa  ajili ya ujenzi wa chuo hicho kitakachokuwa kinatoa fani mbalimbali za ufundi.

Tuesday, October 6th, 2009

A Month in Dar Es Salaam

         

  

  By Dr Zinzin Winkoko,

   PIUMA volunteer doctor

”I am on my second day in Tanzania, I have been studying Kiswahili language, the main language spoken in this country, necessary for me for working in this Country as volunteer medical doctor.

  

I am supposed to study 20 hours according to the schedule for beginner course. Because of the limited time, I could not join to group section which is normally open per period but I have a chance to study in special class.


Therefore, every day but Sunday, I have been studying 3 hours per day. Moreover I decided to extend one extra hour a day, for a total four hours every day, given the short duration of my course…Studying language for four hours in a special class, it is not what you could call it a good method but I have to do when it is happening.

 

It is quite tiring after studying 2 hours because absorbing quality of my brain is becoming poor. Especially, 2 hours lesson after lunch time is a tough job. 

 

According to Tanzanian culture, greeting is very important and the people are proud of greeting before doing anything. So, it has been such a difficult issue for me even to buy drinking water in the early days here.


On the other hand, it really takes me time, the lady doctor who come from Burma (Myanmar), South East Asia, to be ready and not to be shocked when a stranger appear suddenly willing to greet, even though I know the proverb that says “when in Rome do as Romans do!”. I really regret and feel sorry for my late replies to their sincere and friendly greetings!!!

  

Another issue is for the food: I am the one who loves Asian food like papaya salad, other spicy food and Myanmar traditional food called “Mont Hin Khar” . Not only in Myanmar, but also in Thailand I was used to that food for one year. It is hard now to get familiar with African food, especially stiff porridge called “Ugali”. Sweet tea every early morning is a similar custom like in my home town, but those who don’t have that habit still need to be trained.

  

It shouldn’t be left about the bus called “Daladala” when talking about Dar Es Salaam. There are too much crowed in the bus in office hours in my country, but ladies, are first priority usually according to our custom.


We, ladies, old people and children, have been comfortable in the bus while travelling also. Because of cost effectiveness, we have been trying to take the bus from the bus station called “Mwenge” which is not so far from the place we are staying. After waiting for a while, a median size bus that is going to downtown was coming, and there was also crowded in office hour like our country exception with no priority to ladies here. And then, I was really surprised when something was happening unexpectedly, but I was trying to cope with the habits of that city. Somehow, I still like that city.
 

 

Sincerely, I was afraid of dogs since I was in childhood and never imagine staying for one month at the house with six dogs. But finally, these days makes me a part of duty to buy some biscuits for them, to make them friendly. Incredibly they even became some days I would never forget about.

 

After 2 week studying time, I have a chance to practice around the campus such as in shopping center, restaurant and music center around Nyum Ba Ya Sanam which is the place where I used to studying. However, studying one language within 3 weeks made me crazy sometimes, and I did had bad mood on the way back to the place I stayed and even thought I should give up.
But in reality I did not!!!! 

 

Finally, Days passed by very quickly, and I came to the night before I am going to leave for IRINGA . I wish I could come back to that beautiful city to meet with native friends from Dar Es Salaam and wish to chat by Kiswahili.”

zinzin winkoko during her swahil training at Dar Es salaam-Tanzania

zinzin winkoko during her swahil training at Dar Es salaam-Tanzania

 

 

Monday, September 28th, 2009

Barabara Kukarabatiwa

Na Evance Seth

Wilaya ya Makete inaweza ikaepukana na adha ya tatizo sugu la bara bara kufikia mwakani. Hayo yamefahamika mwishoni mwa wiki iliyopita wakati naibu waziri wa miundo mbinu Mh. Hezekia Chibulinje akipokea taarifa ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo akiwa ziarani wilayani Makete.

Akisoma taarifa hiyo mkuu wa wilaya Bi. Hawa Ng’umbi amesema kuwa Halmashauri ya wilaya Makete imekuwa ikipokea fedha kutoka mfuko wa barabara ambazo zimekuwa hazitoshelezi mahitaji halisi ikilinganishwa na urefu wa barabara za Makete.

 

Kufuatia hali hiyo Naibu Waziri wa miundo mbinu alikiri kuwepo kwa tatizo sugu la bara bara wilayani Makete kwa muda mrefu. Hata hivyo Mh. Chibulunje aliwapa matumaini viongozi wa wilaya waliofika kumpokea kwa kuwaambia kuwa serikali imesikia kilio cha wananchi wa Makete kwani barabara za wilaya ya Makete zitapata suruhisho la kudumu.

 

Mheshimiwa Chibulunje alitembelea maeneo kadhaa ya wilaya ya Makete kujionea ubovu wa  Bara bara na utekelezaji wa miradi hiyo. Hata hivyo wananchi kadhaa waliozungumza na mtandao huu walionyesha wasi wasi wa matokeo ya tathmini atakayopata Mheshimiwa naibu waziri wa Miundo mbinu katika ziara yake.

 

Wakizungumza kwa nyakati tofauti wananchi wachache waliohojiwa na mwandishi wetu walisema, kwa ujumla mtu hawezi kuona ubovu mkubwa wa bara bara wilayani makete kama atatembelea wilaya hii wakati wa kiangazi. Wananchi wengi walisema wilaya hii inayozungukwa na milima huwa haipitiki wakati wa masika kutokana na utelezi, matope na mashimo yanayosababishwa na mvua.

 

“angekuja wakati wa masika asikilizie mziki wake” alisema kijana Omega wa Mabehewani Makete akimaanisha mheshimiwa waziri aone ukubwa wa tatizo. “wakati wa masika huwezi kusafiri kwa gari wilayani Makete kwa zaidi ya Kilomita kumi bila kusukuma Gari lako” alimalizia kijana huyo.

 

Wapo wanachi wengine waliosema wanasubiri kuona matokeo ya utekelezaji wa mradi huu ndio watoe pongezi zao kwa naibu waziri na serikali.

Monday, September 28th, 2009

Zoezi la kuandikisha wapiga kura

na Evance Seth

Wananchi wilayani Makete kwa muda wa siku tano mfululizo wameungana na watanzania wenzao wa mkoa wa Iringa kushiriki katika zoezi la kuboresha daftari la kudumu la wapiga kura. Zoezi hili lilimhusu kila mwananchi mwenye umri wa kuanzia miaka kumi na nane na kuendelea  na mwenye akili timamu.

Akiongea na wananchi wa kata ya Iniho Mtendaji wa kata ya Iniho Bw. Christopher Fungo aliwaambia wananchi wa kata hiyo  kuwa umri wa miaka zaidi ya kumia na nane na akili timamu ndio sifa pekee za kumfanya mtu aandikishwe katika daftari la kudumu la wapiga kura

Akifafanua zaidi mtendaji huyo alisema “mtu ambaye hana kadi ya kupigia kura au endepo amepoteza  hataruhusiwi kupiga kura” hata Hivyo alizidi kusema watu wanaofikisha miaka hiyo wataandikishwa na kupewa kadi za kupigia kura na baadaye kuruhusiwa kushiriki katika zoezi la upigaji kura.

Kuhusu wapiga kura waliondikishwa lakini wamefariki mtendaji huoyo alisema kuwa kadi zao zinapswa kurudishwa kwa muandikishaji ili taarifa zao ziweze kufahamika.

Akiongea na mtandao huu mmoja wa wanachama wa PIUMA aliyejiandikisha katika zoezi hili Bw. Shem Kilemile alisema kupiga kura ni haki na niwajibu wa kila raia. “Nikiwa kama raia wa nchi hii nina haki ya kuchagua na kuchaguliwa, na ninaona ni wajibu wangu kutimiza haki hii” alisema Bwana Kilemile.

 

Friday, September 18th, 2009

WANACHAMA WA PIUMA WAALIKWA KUTEMBELEA KIKUNDI CHA CHAKUNIMU – NJOMBE.

 

 

Na Witness Ngumba.

 

Wanachama  watano  wa PIUMA wiki iliyopita walialikwa kwenda Njombe kuonana na kikundi cha CHAKUNIMU(Chama cha Kupambana na UKIMWI ,Nyumbanitu, Itulike, Mvelela, Ulembwe) ili kujifunza  na kubadilishana mawazo juu ya kuhudumia wagonjwa majumbani (HBC) na kujifunza kazi mbalimbali zinazofanya na kikundi hicho.

 

Wanachama hao wameenda kukaa siku kumi (10) na wanachama waliokwenda ni Markusi Chaula, Apolo Mbogela , Esterina Swalo, Anamere Pilla na Sabina Sanga.

 

Akizungumza na mwandishi wa habari hii mkuu wa msafala Bwana Markusi Chaula alisema kuwa matembezi hayo yalikuwa ya siku kumi na tumetembelea vijiji sita vyenye umbali wa kilomita 114,na wagonjwa tuliotembelea ni 84, vijiji vyote hivyo tulikuwa tunatembea kwa mguu.Vijiji vyote hivyo tuliongozwa na Lawrence Lilawola- Mwenyekiti wa CHAKUNIMU na Amoni Msigwa- Katibu wa CHAKUNIMU. Na jumla ya watu liokuwa tumeshiriki katika matembezi haya tulikuwa watu 30 tuliokuwa tumetoka sehemu mbalimbali.

 

Aliendelea kusema kuwa  kazi zinazofanywa na  kikundi cha CHAKUNIMU ni kuhamasisha jamii kwenda kupima Virusi vya Ukimwi kwa hiari, kuwatembelea wagonjwa majumbani katika vijiji vyote vilivyo ndani ya CHAKUNIMU.

 

Lakini kuna baadhi ya tofauti tulizoziona kati ya PIUMA na CHAKUNIMU, CHAKUNIMU ni kukundi cha watu mchanganyiko  waliopima Virusi vya Ukimwi na ambao hawajapima na wakati sisi PIUMA ni kikundi cha tuliopima na tunaishi na Virusi vya Ukimwi  na wao kituo cha kuchukulia dawa ni mbali sana sio sawa na sisi PIUMA. Pia wao hutembelea wagonjwa kila kijiji kilichopo ndani ya CHAKUNIMU wakati sisi PIUMa hatufanyi hivyo.

 

Baada ya kumaliza kutembelea vijiji sita tulikusanyika pamoja na kukaa kikao cha kutathimini kazi ilivyofanyika, wajumbe wa pande zote mbili walisema kuwa tumefanya kazi kubwa kwani watu wengi wamefurahi kuwatembelea  kwani wameelika sana juu yetu kwa kujieleza ni jinsi gani tunavyoishi na VVU na kutualika tena tuweze kuwatembelea kwa wakati mwingine.

 

Wanachama walioenda CHAKUNIMU - NJOMBE

Wanachama walioenda CHAKUNIMU - NJOMBE

 

 

 

 

Thursday, September 10th, 2009

WANAPIUMA WAKUSANYIKA KUMKARIBISHA DR. ZIN ZIN.

 Na Witness ngumba.

 

Juzi tarehe 08/09/2009 ulifanyika Mkutano wa kumkaribisha Dr. zin zin na wanachama wa PIUMA pamoja na uongozi wao, mkutano huo ulifanyikia  kwenye jengo la PIUMA. Jumla ya wanachama waliohudhuria walikuwa 80 idadi hii ni kama nusu ya wanachama wote,  wanachama wengine walishindwa kufika kutokana na sababu mbalimbali walizotoa kwa katibu.

 

Akizungumza na mwandishi wa habari hii Katibu Mkuu wa PIUMA  Bi. Anna Mwinuka “alisema kuwa ujio wa Dr. Zin Zin ni mzuri kwa sababu ameshaanza kufanya kazi na wanaPIUMA kama kuhudumia wagonjwa kwa utafiti wa ndani, hivyo wagonjwa wanaendelea kufarijika na kumiminika kwa kasi kwenda kituoni kupima afya zao kutokana na uwepo wake PIUMA. Amesema kuwa yupo  tayari kutufundisha wanaPIUMA kiingereza pamoja na kuanzika kwa kutumia Kompyuta. Na kwa nyuso za wanachama wengi walionyesha kufurahia ujio wake huyu daktari kwani siku hiyo baada ya kujitambulisha kwa jina la Dr. Zin Zin na kueleza malengo yake ya kuja PIUMA ni kufanya kazi na PIUMA hasa kwenye masuala ya afya, wanachama walifurahi na kuimba nyimbo kwa shangwe na vigelegele.

 

Kwa niaba ya wanaPIUMA wote tunapenda kutoa shukrani zetu kwa wale wote walioshiriki katika mchakato wa kumtafuta daktari huyu na hatimaye kumsafirisha na kufika PIUMA  kwani tumetambua kuwa tunapendwa na wafadhili  na mnautambua umuhimu wa afya zetu”alisema Katibu”.

 

WanaPIUMA wakisubiri mkutano kwenye jengo lao.

WanaPIUMA wakisubiri mkutano kwenye jengo lao.

Dr. zin Zin akizungumza na wanaPIUMA

Dr. zin Zin akizungumza na wanaPIUMA

 

WanaPIUMA wakiimba na kutawanyika.

WanaPIUMA wakiimba na kutawanyika.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

Tuesday, September 1st, 2009

ELIMU NI UFUNGUO WA MAISHA

Na Evance Seth

 

Mwito wa serikali kwa wananchi wa elimu kwa wote umepokelewa kwa mikono miwili na wananchi Katika Wilaya ya Makete. Hayo yameonyeshwa na wananchi wa kijiji cha Ikovokovo waliojenga shule ya msingi iliyoanza tarehe 15 mwezi wa pili mwaka 2002.

Shule hiyo ilianza na wanafunzi hamsini na moja ikiwa na mwalimu Leonard Kyando aliyekuwa mwalimu pekee wa shule hiyo ambaye kwa sasa ni mwalimu mkuu msaidizi.

Akizungumza na mwandishi wa habari hii Bw. Kyando alisema, Mwanzilishi wa wazo ni wananchi toka vitongoji vitatu navyo ni Ikovokovo, Kisiva na Masalala. Shule hii ilianza kwa mtaji wa nguvu za wananchi na kupata msaada uliotolewa na serikali kupitia mpango wa MEM utolewao kwa kila shule kujengewa jengo moja au mawili.

Kwa sasa shule inajumla ya walimu wanne na  wanafunzi mia moja arobaini na moja kati yao wavulana 72 na wasichana 69.Pia shule hiyo inatoa elimu ya watu wazima mara mbili kwa wiki.

“Kwa mtu asiye penda kumpeleka mtoto shule tunampa  elimu na kumshawishi mzazi au mlezi juu ya faida za  elimu kwa mtoto kwa maisha ya baadaye kama akikaidi zaidi anaweza kuchukuliwa hatua za kisheria kama ataendelea kukataa hatampeleka mtoto shule” alisema Bw. Kyando.

Akizungumzia matatizo yanayoikabili shule hiyo, Bw. Kyando kwasasa tatizo la yatima bado ni kubwa kwani wanafunzi 40 ni yatima na 20 wanaishi katika mazingira magumu. “watoto hao hupewa msaada kidogo kama daftari na biki kutoka kwenye mashirika mbalimbali pamoja na walimu” aliongeza Bw. Kyando.

Changamoto  zingine zinazoikabili shule hiyo ni pamoja na ukosefu wa  maji, vyumba vya madarasa , nyumba za walimu ,vifaa vya michezo pamoja na zana za kufundishia.  Walimu wa shule hiyo kwa pamoja walikiri kuwa taaluma kwa ujumla ni nzuri. “Malengo yetu kwa baadaye ni kuboresha taaluma na kuakikisha wanafunzi wote wanafaulu mtihani na kwenda sekondari.” Alisema Mwalimu Sanga 

Wanafunzi wa shule ya Msingi Ikovokovo

Wanafunzi wa shule ya Msingi Ikovokovo

Friday, August 28th, 2009

PIUMA BUIDING TO DATE

slowly we can!

upper floor

upper floor

 

windows and door flem
windows and door flem

Friday, August 28th, 2009

Makete waanza kulima Pareto

Na Evance Seth.

 

Wananchi wilayani Makete wamekuwa na furaha tena baada ya zao la biashara la Pareto kuanza kununuliwa tena. Pareto ni zao pekee la biashara Wilayani Makete  lilitoweka baada ya kukosekana kwa soko.

 

Akizungumza na mwandishi wa habari hii mmoja wa wakulima wa zao hili Bwana Kensi alisema ”Nimeanza kulima zao hili mwaka 2007 baada ya kupata nguvu kutoka kwa  kampuni ya pareto walipokuja kijijini kwetu na kutuahidi soko la uhakika’’

 

Wanunuzi hao wa pareto wanatoa motisha na uhamasishaji kwa wakulima kulima kwa wingi zao hili kwa kuwapunguzia gharama za ukulima kwa kugawa mbegu bure kwa wanakijiji wakulima. Mbegu ambazo zimekuwa zikipatikana kwa watendaji wa vijiji bure hutolewa bila urasimu wote.

 

Bw. Kensi mmiliki wa shamba la ekari moja anavuna pareto yake kila wiki na hutumia siku tatu kukauka wakati wa kiangazi na wiki moja wakati wa msimu wa mvua. Aliendelea kusema bei ya kilo moja ya pareto ni sh. 900/= kwa hiyo kwa mwezi huwa anakusanya kilo zisizopungua arobaini.

 

“Nikishakausha pareto yangu huipeleka kwa Afisa kilimo ambapo hupimwa na kupewa pesa zangu keshi”. Alisema Bw. Kensi.

 

Kilimo cha pareto ni kilimo rahisi sana kwani hakihitaji mbolea na matunzo makubwa zaidi ya palizi inayofanywa mara mbili kwa mwaka. Na zao linalompatia mkulima pesa kila wiki.

 

Hata hivyo Bwana Kensi alisema kuwa matatizo madogo madogo ambayo huwa anayapata hasa wakati wa masika pareto hukuchukua muda mrefu kukauka kwani jua huwa linakuwa la shida, na mvua zikinyesha mfululizo husababisha pareto hiyo kuoza, na biashara yake kuwa sio nzuri.

 

‘’Pamoja na kuwa biashara sio nzuri malengo yangu ya baadaye ni kuongeza kulima mashamba mengine ya pareto, kwani pesa ninayopata inanikwamua kwenye matatizo madogo madogo ya kifamilia”alisema Bw. Kensi.

 

Ulimaji wa zao la preto ulistawi kuanzia miaka ya 1960 na kusimama miaka ya 1980 baada ya matumizi ya DDT kupigwa marufuku na hivyo pareto ambayo ilikuwa malighafi ya dawa hiyo kukosa soko.

 

Ingawa wakulima wa Makete hawajui pareto inatumika kwa ajili ya nini sasa, lakini wanashukuru kwasababu hivi sasa soko la Pareto limekuwa zuri kwani imeshaanza kupata soko kwenye soko la dunia.

Bwana Kensi akiwa anachuma pareto.

Bwana Kensi akiwa anachuma pareto.