Latest News

February 23rd, 2010

Watoto Yatima.

Na Evance Seth.

 

Jamii  imeshauriwa  kuwa na moyo wa kutoa  vitu mbalimbali  kwa watoto yatima  wanao lelewa katika vituo mbalimbali ili kuwa fariji  na wao kuto kuona  kama jamii imewasahau.

 

Rai hiyo imetolewa na mkuu wa wilaya ya Makete  Mh. Hawa Ng’humbi  wakati akikabidhi  msaada wa vitu mbalimbali wenye thamani  zaidi  ya shilingi laki moja  kwa watoto wa kituo cha yatima  cha Bulongwa  Lengo la ziara yake hiyo  ni kuona  kituo hicho  pamoja kuelewa  historia yake  na kuelewa kinaendeshwaje.

 

Akipokea  msaada wa vitu hivyo  mmoja wa watumishi  wa kituo hicho  amesema kituo hicho  kinahitaji msaada mkubwa  wa watu wa serikari  kwa ujumla  ili kiweze kujiendesha chenyewe kwani kwa sasa kinamtegemea  mzungu  mmoja  ambaye kwa sasa ni mzee anayeitwa  SISTER ANNA.

 

Mh.  Mkuu wa wilaya  pia aliwafariji watoto wanaolelewa  katika kituo hicho  ambacho kina watoto thelathini na miongoni  mwao  watoto sita  wanaishi na virusi vya UKIMWI

 

Katika ziara hiyo mkuu wa wilaya  aliongozana  na  Diwani wa kata ya Bulongwa Bw. Estomih Mahenge, M/K  umojwa wa wanawake Tanzania wilaya ya Makete   na Bi. Erika Sanga,  pamoja na  Israel Green  Kutoka  kituo cha polisi  makete.

 

February 23rd, 2010

Ujenzi wa Zahanati Unyagala.

 

Na Evance Seth.

 

Zaidi ya shilingi milioni hamsini na saba  pointi  nane zinatarajia kutumika  kwa ajili ya ujenzi wa  zahanati ya Unyangala   na Igumbilo  katika kipindi cha  mwaka  2009-2010 wilayani Makete.

Akizungumza  mratibu wa  mfuko wa maendeleo  ya jamii  wilayani Makete  Bi Jaklini Mroso  ameeleza kuwa fedha hizo  zitatumika kwa ajili ya ununuzi  wa vifaa vya ujenzi  pamoja na nguvu za wananchi  zitahitajika  kukamilisha miradi  hiyo kwa wakati.

Naye katibu wa  zahanati ya Unyangala  Bw. Boaz Sanga   pamoja na mtunza hazina  Bw. Erasto Mvela wamesema  kuwa msaada huo  umekuja kwa wakati  kwao kwani wamekuwa wakitumia muda mwingi  kuwa peleka wagonjwa  katika  zahanati ya Utengule ambapo ni mbali.

Mfuko wa maendeleo ya jamii   TASAF  wilayani Makete  umekuwa mkombozi  kwa wananchi wengi  wilayani Makete hasa vijijini kwa kusaidia misaada mbalimbali ambayo wamekuwa wakiibua  kupitia mikutano ya hadhara, aidha kufuatia hali , katibu  wa mradi  wa ujenzi  wa zahanati  Igumbilo  Bw. Godfrey Sanga  ameeleza  kuwa zahanati hiyo  kwa sasa ipo hatua ya mwisho na ameshukuru  TASAF kwa ufaddhili  wa mradi  huo  na  amewataka wananchi  kuendelea kuunga mkono  jitihada  zinazo fanywa  na TASAF  wilayani makete.

 

 

February 22nd, 2010

Mnada wa Ng’ombe.

 

Na Evance Seth.

 

Mnada wa mifugo  uliopo katika kijiji cha isapulano kata ya  Iwawa  ulioanza kujengwa mwaka  2009-2010 kwa ufadhili wa DADS   NA  DADPS  pamoja na nguvu za wananchi  ulioghalimu kiasi cha  shilingi  milioni kumi na nne na thelathini na nane elfu  14,380,000 umezinduliwa .

Uzinduzi wa mnada huo  umefanywa na mgeni rasimi  ambaye  ni mbunge wa wilaya ya makete MH BINILITI SAATANO MAHENGE  ambapo amewatakia wananchi  wa kijiji cha Isapulano na wananchi wa wilaya  makete  kwa ujumla kuutumia  mnada huo  ili kujiongezea kipato.

Aidha ameendelea kusema wananchi wote wanatakiwa  kuonesha upendo kwa wageni  watokao nje ya makete kwa kuto wakatisha tama kwa kuwaibia mali zao pindi  wanapo kuja kwenye mnada huo. Na  ameeleza mafanikio yaliyo patikana katika  awam ya nne ya uongozi  kwa kipindi cha miaka mitatu na nusu  kwa wakazi wa wilaya ya makete  ambayo ni kufufua  zao la pareto pamoja na elimu ambapo kila kata  kumejengwa  shule za sekondari na wanafunzi wengi kufanikiwa kujiunga na elimu ya sekondari.

Katika sherehe za uzinduzi wa mnada huo MH mahenge aliongozana na mwenyekiti  wa Halmashauri  wa wilaya ya makete  ambaye pia  ni diwani wa kata ya Iwawa MH ONO SIKUNALA NKWAMA , mtendaji  Iwawa  KIWONE ,  AFISA KILIMO NA MIFUGO WA WILAYA BW ERNEST MKONGO pamoja na watalam wake.  Aidha changamoto kubwa  inayo ukabili mnada huo  ubovu wa barabara inayotoka  makete kwenda kijiji hapo ambayo wakati  wa masika haipitiki kwa uraisi pamoja na ukosefu wa miundo mbinu ya maji ambapo  kwa suala  la maji MH ONA nkwama ametoa liri mbili za bomba kwa ajili ya kusogeza  maji eneo la mnada  na suala  barabara kuahidi kushughulikia  ipitike muda wote.

 

Wakiongea kwa nyakati tofauti  wananchi wa kijiji hicho  wameonekana kufurahishwa na  na mnada ambao  utakuwa ukifanyika  mara mbili kwa mwezi tarehe kumi na tano na tarehe thelathini ya kila mwezi na kusema mifugo yote itauzwa  mnadani  ili kupata soko la uhakika  na si  la kuuzia mitaani.

 

                                    

February 22nd, 2010

Semina ya usimamizi wa mitihani ya darasa la Saba.

 

Na Evance Seth

 

Semina ya maelekezo  kuhusu  usimamizi wa mtihani  wa taifa  wa kuhitimu elimu ya msingi iliyo fanyika  katika  ukumbi wa Halimashauri ya wilaya ya makete.

 

Akinzungumza katika semina hiyo mkuu wa wilaya ya makete Bi HANA HUMBI  amesema  wasimamizi wanatakiwa  kuepuka vishawishi  kama vile rushwa  katika  zoezi hilo la usimamizi.

Alisema kuwapa watoto mtihani au majibu  ni kujenga  Taifa lenye watu wajinga  wasio na elimu wala  taaluma na kusema  yeyote atakaye gundulika  kufanya hivyo  atawajibika kisheria.

Akifunga semina hiyo Mkurugenzi  wa Halmashauri ya wilaya ya makete  Bi IMELDA ISHUZA  ametaka wasimamizi hao wa mtihani kuwa na upendo  kwa watoto  kwa kuwaelekeza vizuri  pale wanapo hitaji msaada  wa msimamizi.

 

February 22nd, 2010

Mafunzo ya CUAMM.

 

 Na Evance Seth

 

Katika wilaya ya makete  kuna shirika moja lisilo la kiserikali linaloitwa CUAMM linalotokea mkoani Iringa.

 

Shirika hilo linajishughulisha na  mambo  ya upimaji VCT . Na shirika hilo liliomba kufanya  kazi na mashirika mengine yaliyopo katika wilaya ya makete yanayo jishughulisha  na  mambo ya upimaji.

 

Pia shirika hilo lilitoa mafunzo  mbalimbali yakiwemo mafunzo ya;

1. UANDIKAJI WA RASMU NA MRADI

2. UTAFUTAJI WA VYANZO VYA FEDHA

3. UFUATILIAJI  NA TATHIMINI

 

Mashirika yaliyo shiliki mafunzo hayo ni1.MAKEYODENI , PIUMA, MAWATA5, LCCB, FEMA, IDYDC, SUMASESU, MAHEPO na  MASUPHA.

Na kila shirika liliwakilisha viongozi wane. Na mafundisho hayo  yaliendeshwa  na  WILLIAM YOTHAM -    UNV   na ABRAHAM   SANGA - CHAC.

 

Na  mafunzo hayo  yalifungwa na FLORA  NSEMWA  toka shirika la CUAMM  na kuagana  na kutakiana safari njema pamoja na utendaji wa kazi njema.

 

February 17th, 2010

Mtandao wa vijana Makete.

 

Na Evance Seth.

 

Katika Wilaya ya Makete kuna mtandao  mmoja unajishughulisha na vijana unaojulikana kwa jina la MAKEYODEN.

 

Mtandao huo uliamua kufanya kikao cha viongozi wa mtandao tarehe 22/01/2010 na kujadili malengo mbalimbali ya kufanya  2010-2013, na malengo hayo ni kama

 

1.KUBORESHA UONGOZI  ni kufanya marekebisho katiba ya makeyoden, kuandika sera kanuni na taratibu za makeyoden, kanuni za utendaji na uendeshaji , kanuni na taratibu za fedha na kanuni za ustawi na mahusiano na kuendesha vikao vya kamati kuu na mkutano mkuu.

 

2.KUBORESHA UTENDAJI ni kuajili watendaji wa ofisi kuu, kumaliza  ujenzi wa ofisi ya mtandao na vituo vya kata, kununua  samani  na vitendea kazi, kuendesha vikao vya utendaji na  kuanzisha tovuti na internet  ya makeyoden.

 

3.KUBORESHA  MAHUSIANO NA USHIRIKIANO BAINA YA MAKEYODEN NA WADAU WENGINE  ni kuandaa utambulisho wa  shughuli za makeyoden kuandaa orodha ya  wadau mbalimbali, kusambaza utambulisho wa makeyoden kwa njia mbalimbali na kuhudhulia matukio  ya wadau mbalimbali.

 

4.KUENDELEZA SHUGHULI ZA MAKEYODENI ZILIZOPO ni kuhimiza  umaliziaji wa vituo vya kata  tisa , kusaidia vituo saba vilivyokamilika vianze vianze utekelezaji wa mipango na  kukamilisha  usajili wa redio na kutayarisha mpango wa kazi na wa  kujitegemea  wa redio na kuongeza  nguvu  ya kudhibiti maambukizi dhidi ya ukimwi.

 

Kikao hicho kilifanyika  na viongozi wa mtandao  ambao  ni

1.       NAHAMAN SANGA  - MWENYEKITI

2.       JUMA  SINENE  - KATIBU

3.       EMANUEL SANGA  - MWASIBU

4.       FRANCISKO  SIGARA - MJUMBE

5.       SALEHE  NGULO  - MJUMBE

 

Na mwisho viongozi hao walihitimisha kikao  kuagana na kutakiana safari njema.

 

January 25th, 2010

PIUMA waanza kutembelea vijijini.

 

Na Witness Ngumba.

 

Viongozi wa PIUMA pamoja na baadhi ya wanachama wa PIUMA wiki iliyopita walitembelea kijiji cha Utanziwa kwa ajili ya kuwatembelea wanachama wa PIUMA wanaoishi katika kijiji hicho.

 

Zoezi hili liliongozwa na Katibu Mkuu wa PIUMA pamoja na Mwenyekiti,  Daktari Zin zin, na wanachama wawili ambao ni Izack Sanga na John Nyivaha.

 

Kazi ambazo walikwenda kuzifanya ni pamoja na;

·         kuwasajili wanachama waliokuwepo kwa upya kwa kuzingatia vipengele vifuatavyo, kuhakikisha kila mwanachama yumo kwenye orodha ya wanachama hai na waliopiga picha.

·         Kutoa ushauri nasaha kwa wasio wanachama ili wajiunge na shirika la PIUMA kwa ajili ya kupata huduma zinazotolewa na shirika.

·         Kujua maendeleo ya wanachama kiafya na kwa wale wanaoumwa wapewe huduma inayostahili.

·         kwa wale ambao walikuja kwenye zoezi hilo waliombwa kuwaambia wenzao kuwa wafike ofisini ili waweze kupigwa picha kwa ajili ya vitambulisho.

Kwa wale ambao walishindwa kufika kwenye kituo  tulichokuwa tumekusanyikia kutokana na afya zao kuwa mbaya tulihakikisha tunawetembelea majumbani kwao ili kuwajulia hali na kuwapa ushauri. Zoezi hili litaendelea kwa kila wiki kwa kijiji kimoja mpaka tutakapomaliza vijiji vyote “alisema Katibu Bi. Anna Mwinuka”

Timu ya wanaPIUMA wanaotembelea vijijini

Timu ya wanaPIUMA wanaotembelea vijijini

 

 

 

 

 

January 6th, 2010

Mkutano mkuu wa mwaka PIUMA.

Na Witness Ngumba.

Mkutano mkuu wa mwaka wa PIUMA umefanika tarehe 18/12/2009, mgeni rasmi wa mkutano alikuwa ni Mkuu wa Wilaya Bi. Hawa Ng’humbi, wageni wengine waliokuwepo ni pamoja na Joseph Chaula – DAS, Felician Chawala  - Ag. DMO, Hamza – ofisi ya DSO, Erica Sanga – Viti maalumu, Estomih Mahenge – Diwani bulongwa, Ambikile Mwaihola – Afisa Tarafa, Clemence – WEO Bulongwa, Edward Masevela – Ad. BLH, Benitho Ngailo - MASUPHA wanachama wa PIUMA waliokuwa wamehudhuria walikuwa 75  na wengine wengi.

Ilisomwa taarifa ya Katibu na Katibu mkuu pamoja na taarifa ya fedha ilisomwa na Mtunza Hazina wa PIUMA.

Mkuu wa Wilaya alitoa salamu na shukrani nyingi kwa shirika la PIUMA kwa kazi nyingi zinazofanywa na shirika hili hasa  dhidi ya mapambano ya UKIMWI. Aliendelea kusema kuwa alipokuwa alifika katika Wilaya ya Makete shirika ambalo limekuwa likijishughulisha na masuala ya upimaji ni shirika la PIUMA , aliwaasa wanachama wa PIUMA kuendelea kutoa elimu kwa jamii juu ya faida za kupima pamoja na hasara za kutokupima afya zao.

Pamoja na hayo Mkuu wa Wilaya alishukuru kwa ujenzi wa jengo la PIUMA ambalo tunategemea kuwa litakuwa Zahanati ya PIUMA hapo baadaye na kuwaahidi kuwa atachangia kiasi cha sh. 200,000/= kwa ajili ya ujenzi wa jengo la PIUMA.

 

wanachama wa PIUMA wakiwa kwenye mkutano

wanachama wa PIUMA wakiwa kwenye mkutano

 

Mkuu wa Wilaya Bi. Hawa Ng'humbi akitoa hotuba

Mkuu wa Wilaya Bi. Hawa Ng'humbi akitoa hotuba

 

Katibu mkuu akisoma taarifa ya mwaka.

Katibu mkuu akisoma taarifa ya mwaka.

 

Ag. DMO akitoa salamu.

Ag. DMO akitoa salamu.

 

DAS- Makete akitoa salamu

DAS- Makete akitoa salamu

December 21st, 2009

Wanachama wa PIUMA wakifanya usafi kwenye jengo lao.

Na Witness Ngumba

 

Wanachama wa PIUMA wiki iliyopita walikuwa wanafanya usafi kwenye jengo lao kwa ajili ya maandalizi ya mkutano mkuu wa mwaka.

 

Akizungumza katibu mkuu Bi. Anna Mwinuka alisema kuwa usafi utafanywa na wanachama walio katika vijiji vya karibu na jengo. Jumla ya wanachama waliofika kwenye usafi walikuwa 17

 

Usafi uliofanyika ulikuwa ni ndani ya jengo na usafi wa nje ya jengo utafanywa kwa siku nyingine na wanachama wote wa PIUMA baada ya jengo lote kuisha.

 

 

 

WanaPIUMA wakifanya usafi

WanaPIUMA wakifanya usafi

Dr. zin zin nae akiwa ndani ya usafi

Dr. zin zin nae akiwa ndani ya usafi

Afisa mtendaji nae akiwa ndani ya kazi

Afisa mtendaji nae akiwa ndani ya kazi

December 3rd, 2009

Siku ya UKIMWI duniani 1.12.2009

Na Witness Ngumba

Siku ya UKIMWI duniani ni siku ambayo huwa inaadhimishwa kila mwaka Tanzania nzima kwa ajili ya kuwakumbuka watu waliokufa kwa ugonjwa wa UKIMWI pamoja na wanaoishi na Virusi vya UKIMWI.

 

Kwa Wilaya ya Makete Tarafa  ya Bulongwa Siku hii  imeadhimishwa katika tarafa ya Bulongwa kijiji cha kitula ikiwa ni muunganiko wa kata mbili, kata ya Kipagalo na kata Bulongwa. Sherehe hii ilianza rasmi saa 6:00 mchana ikiongozwa na katibu Tarafa wa Bulongwa Bw. Ambikile Mwaihola, Mgeni rasmi wa sherehe hii alikuwa ni Mh. Diwani Estomih Mahenge. Kauli mbiu ya mwaka huu ilikuwa “UHURU NI UWEZO

 

Mgeni rasmi aliwashukuru watu wote wanaoishi na Virusi vya UKIMWI kwa kufuata taratibu zote za dawa pamoja na mashirika yanayosaidia kutoa huduma ikiwemo PIUMA.

Katika sherehe hii PIUMA waliandaa kwaya, igizo pamoja na kugombea umiss Uhuru Bulongwa, aliyeongoza kwa umiss alikuwa ni Rehema Nyamule, akifuatiwa na  Wema Sanga, Anna Mwinuka,Tulingila Sanga.

Mh. Diwani akitoa zawadi kwa mamiss PIUMA

Mh. Diwani akitoa zawadi kwa mamiss PIUMA

 

 

 Miss uhuru PIUMA 2009 ni Rehema nyamule.

Miss uhuru PIUMA 2009 ni Rehema nyamule.