February 23rd, 2010
Na Evance Seth.
Jamii imeshauriwa kuwa na moyo wa kutoa vitu mbalimbali kwa watoto yatima wanao lelewa katika vituo mbalimbali ili kuwa fariji na wao kuto kuona kama jamii imewasahau.
Rai hiyo imetolewa na mkuu wa wilaya ya Makete Mh. Hawa Ng’humbi wakati akikabidhi msaada wa vitu mbalimbali wenye thamani zaidi ya shilingi laki moja kwa watoto wa kituo cha yatima cha Bulongwa Lengo la ziara yake hiyo ni kuona kituo hicho pamoja kuelewa historia yake na kuelewa kinaendeshwaje.
Akipokea msaada wa vitu hivyo mmoja wa watumishi wa kituo hicho amesema kituo hicho kinahitaji msaada mkubwa wa watu wa serikari kwa ujumla ili kiweze kujiendesha chenyewe kwani kwa sasa kinamtegemea mzungu mmoja ambaye kwa sasa ni mzee anayeitwa SISTER ANNA.
Mh. Mkuu wa wilaya pia aliwafariji watoto wanaolelewa katika kituo hicho ambacho kina watoto thelathini na miongoni mwao watoto sita wanaishi na virusi vya UKIMWI
Katika ziara hiyo mkuu wa wilaya aliongozana na Diwani wa kata ya Bulongwa Bw. Estomih Mahenge, M/K umojwa wa wanawake Tanzania wilaya ya Makete na Bi. Erika Sanga, pamoja na Israel Green Kutoka kituo cha polisi makete.
Posted in News | 1 Comment »
February 23rd, 2010
Na Evance Seth.
Zaidi ya shilingi milioni hamsini na saba pointi nane zinatarajia kutumika kwa ajili ya ujenzi wa zahanati ya Unyangala na Igumbilo katika kipindi cha mwaka 2009-2010 wilayani Makete.
Akizungumza mratibu wa mfuko wa maendeleo ya jamii wilayani Makete Bi Jaklini Mroso ameeleza kuwa fedha hizo zitatumika kwa ajili ya ununuzi wa vifaa vya ujenzi pamoja na nguvu za wananchi zitahitajika kukamilisha miradi hiyo kwa wakati.
Naye katibu wa zahanati ya Unyangala Bw. Boaz Sanga pamoja na mtunza hazina Bw. Erasto Mvela wamesema kuwa msaada huo umekuja kwa wakati kwao kwani wamekuwa wakitumia muda mwingi kuwa peleka wagonjwa katika zahanati ya Utengule ambapo ni mbali.
Mfuko wa maendeleo ya jamii TASAF wilayani Makete umekuwa mkombozi kwa wananchi wengi wilayani Makete hasa vijijini kwa kusaidia misaada mbalimbali ambayo wamekuwa wakiibua kupitia mikutano ya hadhara, aidha kufuatia hali , katibu wa mradi wa ujenzi wa zahanati Igumbilo Bw. Godfrey Sanga ameeleza kuwa zahanati hiyo kwa sasa ipo hatua ya mwisho na ameshukuru TASAF kwa ufaddhili wa mradi huo na amewataka wananchi kuendelea kuunga mkono jitihada zinazo fanywa na TASAF wilayani makete.
Posted in News | 1 Comment »
February 22nd, 2010
Na Evance Seth.
Mnada wa mifugo uliopo katika kijiji cha isapulano kata ya Iwawa ulioanza kujengwa mwaka 2009-2010 kwa ufadhili wa DADS NA DADPS pamoja na nguvu za wananchi ulioghalimu kiasi cha shilingi milioni kumi na nne na thelathini na nane elfu 14,380,000 umezinduliwa .
Uzinduzi wa mnada huo umefanywa na mgeni rasimi ambaye ni mbunge wa wilaya ya makete MH BINILITI SAATANO MAHENGE ambapo amewatakia wananchi wa kijiji cha Isapulano na wananchi wa wilaya makete kwa ujumla kuutumia mnada huo ili kujiongezea kipato.
Aidha ameendelea kusema wananchi wote wanatakiwa kuonesha upendo kwa wageni watokao nje ya makete kwa kuto wakatisha tama kwa kuwaibia mali zao pindi wanapo kuja kwenye mnada huo. Na ameeleza mafanikio yaliyo patikana katika awam ya nne ya uongozi kwa kipindi cha miaka mitatu na nusu kwa wakazi wa wilaya ya makete ambayo ni kufufua zao la pareto pamoja na elimu ambapo kila kata kumejengwa shule za sekondari na wanafunzi wengi kufanikiwa kujiunga na elimu ya sekondari.
Katika sherehe za uzinduzi wa mnada huo MH mahenge aliongozana na mwenyekiti wa Halmashauri wa wilaya ya makete ambaye pia ni diwani wa kata ya Iwawa MH ONO SIKUNALA NKWAMA , mtendaji Iwawa KIWONE , AFISA KILIMO NA MIFUGO WA WILAYA BW ERNEST MKONGO pamoja na watalam wake. Aidha changamoto kubwa inayo ukabili mnada huo ubovu wa barabara inayotoka makete kwenda kijiji hapo ambayo wakati wa masika haipitiki kwa uraisi pamoja na ukosefu wa miundo mbinu ya maji ambapo kwa suala la maji MH ONA nkwama ametoa liri mbili za bomba kwa ajili ya kusogeza maji eneo la mnada na suala barabara kuahidi kushughulikia ipitike muda wote.
Wakiongea kwa nyakati tofauti wananchi wa kijiji hicho wameonekana kufurahishwa na na mnada ambao utakuwa ukifanyika mara mbili kwa mwezi tarehe kumi na tano na tarehe thelathini ya kila mwezi na kusema mifugo yote itauzwa mnadani ili kupata soko la uhakika na si la kuuzia mitaani.
Posted in News | No Comments »
February 22nd, 2010
Na Evance Seth
Semina ya maelekezo kuhusu usimamizi wa mtihani wa taifa wa kuhitimu elimu ya msingi iliyo fanyika katika ukumbi wa Halimashauri ya wilaya ya makete.
Akinzungumza katika semina hiyo mkuu wa wilaya ya makete Bi HANA HUMBI amesema wasimamizi wanatakiwa kuepuka vishawishi kama vile rushwa katika zoezi hilo la usimamizi.
Alisema kuwapa watoto mtihani au majibu ni kujenga Taifa lenye watu wajinga wasio na elimu wala taaluma na kusema yeyote atakaye gundulika kufanya hivyo atawajibika kisheria.
Akifunga semina hiyo Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya makete Bi IMELDA ISHUZA ametaka wasimamizi hao wa mtihani kuwa na upendo kwa watoto kwa kuwaelekeza vizuri pale wanapo hitaji msaada wa msimamizi.
Posted in News | No Comments »
February 22nd, 2010
Na Evance Seth
Katika wilaya ya makete kuna shirika moja lisilo la kiserikali linaloitwa CUAMM linalotokea mkoani Iringa.
Shirika hilo linajishughulisha na mambo ya upimaji VCT . Na shirika hilo liliomba kufanya kazi na mashirika mengine yaliyopo katika wilaya ya makete yanayo jishughulisha na mambo ya upimaji.
Pia shirika hilo lilitoa mafunzo mbalimbali yakiwemo mafunzo ya;
1. UANDIKAJI WA RASMU NA MRADI
2. UTAFUTAJI WA VYANZO VYA FEDHA
3. UFUATILIAJI NA TATHIMINI
Mashirika yaliyo shiliki mafunzo hayo ni1.MAKEYODENI , PIUMA, MAWATA5, LCCB, FEMA, IDYDC, SUMASESU, MAHEPO na MASUPHA.
Na kila shirika liliwakilisha viongozi wane. Na mafundisho hayo yaliendeshwa na WILLIAM YOTHAM - UNV na ABRAHAM SANGA - CHAC.
Na mafunzo hayo yalifungwa na FLORA NSEMWA toka shirika la CUAMM na kuagana na kutakiana safari njema pamoja na utendaji wa kazi njema.
Posted in News | No Comments »
February 17th, 2010
Na Evance Seth.
Katika Wilaya ya Makete kuna mtandao mmoja unajishughulisha na vijana unaojulikana kwa jina la MAKEYODEN.
Mtandao huo uliamua kufanya kikao cha viongozi wa mtandao tarehe 22/01/2010 na kujadili malengo mbalimbali ya kufanya 2010-2013, na malengo hayo ni kama
1.KUBORESHA UONGOZI ni kufanya marekebisho katiba ya makeyoden, kuandika sera kanuni na taratibu za makeyoden, kanuni za utendaji na uendeshaji , kanuni na taratibu za fedha na kanuni za ustawi na mahusiano na kuendesha vikao vya kamati kuu na mkutano mkuu.
2.KUBORESHA UTENDAJI ni kuajili watendaji wa ofisi kuu, kumaliza ujenzi wa ofisi ya mtandao na vituo vya kata, kununua samani na vitendea kazi, kuendesha vikao vya utendaji na kuanzisha tovuti na internet ya makeyoden.
3.KUBORESHA MAHUSIANO NA USHIRIKIANO BAINA YA MAKEYODEN NA WADAU WENGINE ni kuandaa utambulisho wa shughuli za makeyoden kuandaa orodha ya wadau mbalimbali, kusambaza utambulisho wa makeyoden kwa njia mbalimbali na kuhudhulia matukio ya wadau mbalimbali.
4.KUENDELEZA SHUGHULI ZA MAKEYODENI ZILIZOPO ni kuhimiza umaliziaji wa vituo vya kata tisa , kusaidia vituo saba vilivyokamilika vianze vianze utekelezaji wa mipango na kukamilisha usajili wa redio na kutayarisha mpango wa kazi na wa kujitegemea wa redio na kuongeza nguvu ya kudhibiti maambukizi dhidi ya ukimwi.
Kikao hicho kilifanyika na viongozi wa mtandao ambao ni
1. NAHAMAN SANGA - MWENYEKITI
2. JUMA SINENE - KATIBU
3. EMANUEL SANGA - MWASIBU
4. FRANCISKO SIGARA - MJUMBE
5. SALEHE NGULO - MJUMBE
Na mwisho viongozi hao walihitimisha kikao kuagana na kutakiana safari njema.
Posted in News | 1 Comment »
January 25th, 2010
Na Witness Ngumba.
Viongozi wa PIUMA pamoja na baadhi ya wanachama wa PIUMA wiki iliyopita walitembelea kijiji cha Utanziwa kwa ajili ya kuwatembelea wanachama wa PIUMA wanaoishi katika kijiji hicho.
Zoezi hili liliongozwa na Katibu Mkuu wa PIUMA pamoja na Mwenyekiti, Daktari Zin zin, na wanachama wawili ambao ni Izack Sanga na John Nyivaha.
Kazi ambazo walikwenda kuzifanya ni pamoja na;
· kuwasajili wanachama waliokuwepo kwa upya kwa kuzingatia vipengele vifuatavyo, kuhakikisha kila mwanachama yumo kwenye orodha ya wanachama hai na waliopiga picha.
· Kutoa ushauri nasaha kwa wasio wanachama ili wajiunge na shirika la PIUMA kwa ajili ya kupata huduma zinazotolewa na shirika.
· Kujua maendeleo ya wanachama kiafya na kwa wale wanaoumwa wapewe huduma inayostahili.
· kwa wale ambao walikuja kwenye zoezi hilo waliombwa kuwaambia wenzao kuwa wafike ofisini ili waweze kupigwa picha kwa ajili ya vitambulisho.
Kwa wale ambao walishindwa kufika kwenye kituo tulichokuwa tumekusanyikia kutokana na afya zao kuwa mbaya tulihakikisha tunawetembelea majumbani kwao ili kuwajulia hali na kuwapa ushauri. Zoezi hili litaendelea kwa kila wiki kwa kijiji kimoja mpaka tutakapomaliza vijiji vyote “alisema Katibu Bi. Anna Mwinuka”

Timu ya wanaPIUMA wanaotembelea vijijini


Posted in News | 4 Comments »
January 6th, 2010
Na Witness Ngumba.
Mkutano mkuu wa mwaka wa PIUMA umefanika tarehe 18/12/2009, mgeni rasmi wa mkutano alikuwa ni Mkuu wa Wilaya Bi. Hawa Ng’humbi, wageni wengine waliokuwepo ni pamoja na Joseph Chaula – DAS, Felician Chawala - Ag. DMO, Hamza – ofisi ya DSO, Erica Sanga – Viti maalumu, Estomih Mahenge – Diwani bulongwa, Ambikile Mwaihola – Afisa Tarafa, Clemence – WEO Bulongwa, Edward Masevela – Ad. BLH, Benitho Ngailo - MASUPHA wanachama wa PIUMA waliokuwa wamehudhuria walikuwa 75 na wengine wengi.
Ilisomwa taarifa ya Katibu na Katibu mkuu pamoja na taarifa ya fedha ilisomwa na Mtunza Hazina wa PIUMA.
Mkuu wa Wilaya alitoa salamu na shukrani nyingi kwa shirika la PIUMA kwa kazi nyingi zinazofanywa na shirika hili hasa dhidi ya mapambano ya UKIMWI. Aliendelea kusema kuwa alipokuwa alifika katika Wilaya ya Makete shirika ambalo limekuwa likijishughulisha na masuala ya upimaji ni shirika la PIUMA , aliwaasa wanachama wa PIUMA kuendelea kutoa elimu kwa jamii juu ya faida za kupima pamoja na hasara za kutokupima afya zao.
Pamoja na hayo Mkuu wa Wilaya alishukuru kwa ujenzi wa jengo la PIUMA ambalo tunategemea kuwa litakuwa Zahanati ya PIUMA hapo baadaye na kuwaahidi kuwa atachangia kiasi cha sh. 200,000/= kwa ajili ya ujenzi wa jengo la PIUMA.

wanachama wa PIUMA wakiwa kwenye mkutano

Mkuu wa Wilaya Bi. Hawa Ng'humbi akitoa hotuba

Katibu mkuu akisoma taarifa ya mwaka.

Ag. DMO akitoa salamu.

DAS- Makete akitoa salamu
Posted in News | 3 Comments »
December 21st, 2009
Na Witness Ngumba
Wanachama wa PIUMA wiki iliyopita walikuwa wanafanya usafi kwenye jengo lao kwa ajili ya maandalizi ya mkutano mkuu wa mwaka.
Akizungumza katibu mkuu Bi. Anna Mwinuka alisema kuwa usafi utafanywa na wanachama walio katika vijiji vya karibu na jengo. Jumla ya wanachama waliofika kwenye usafi walikuwa 17
Usafi uliofanyika ulikuwa ni ndani ya jengo na usafi wa nje ya jengo utafanywa kwa siku nyingine na wanachama wote wa PIUMA baada ya jengo lote kuisha.

WanaPIUMA wakifanya usafi

Dr. zin zin nae akiwa ndani ya usafi

Afisa mtendaji nae akiwa ndani ya kazi
Posted in News | 1 Comment »
December 3rd, 2009
Na Witness Ngumba
Siku ya UKIMWI duniani ni siku ambayo huwa inaadhimishwa kila mwaka Tanzania nzima kwa ajili ya kuwakumbuka watu waliokufa kwa ugonjwa wa UKIMWI pamoja na wanaoishi na Virusi vya UKIMWI.
Kwa Wilaya ya Makete Tarafa ya Bulongwa Siku hii imeadhimishwa katika tarafa ya Bulongwa kijiji cha kitula ikiwa ni muunganiko wa kata mbili, kata ya Kipagalo na kata Bulongwa. Sherehe hii ilianza rasmi saa 6:00 mchana ikiongozwa na katibu Tarafa wa Bulongwa Bw. Ambikile Mwaihola, Mgeni rasmi wa sherehe hii alikuwa ni Mh. Diwani Estomih Mahenge. Kauli mbiu ya mwaka huu ilikuwa “UHURU NI UWEZO”
Mgeni rasmi aliwashukuru watu wote wanaoishi na Virusi vya UKIMWI kwa kufuata taratibu zote za dawa pamoja na mashirika yanayosaidia kutoa huduma ikiwemo PIUMA.
Katika sherehe hii PIUMA waliandaa kwaya, igizo pamoja na kugombea umiss Uhuru Bulongwa, aliyeongoza kwa umiss alikuwa ni Rehema Nyamule, akifuatiwa na Wema Sanga, Anna Mwinuka,Tulingila Sanga.



Mh. Diwani akitoa zawadi kwa mamiss PIUMA

Miss uhuru PIUMA 2009 ni Rehema nyamule.

Posted in News | 3 Comments »